-
Marekani, mwanzishaji na msababishaji halisi wa kuvurugika amani na usalama katika Bahari Nyekundu
Feb 07, 2024 03:30Makundi ya Muqawama na nchi zenye misimamo huru katika Asia Magharibi zinaendelea kukabiliana na Mhimili wa Uovu wa Marekani na Israel katika eneo hilo na Bahari Nyekundu katika hali ambayo, kwa kuendeleza uingiliaji wao wa kijeshi, Washington na waitifaki wake wamekuwa ndio waanzishaji na wasababishaji halisi wa kuvurugika amani na usalama katika eneo hilo la Asia Magharibi.
-
Umoja wa Mataifa walaani njama za kuichafua UNRWA
Feb 06, 2024 22:52Maripota wa Umoja wa Mataifa wametangaza kuwa, wanalaani vikali jaribio lolote la kuharamisha na kulichafua Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu la kutolewa pigo kali la mataifa ya Kiislamu dhidi ya Israel
Feb 06, 2024 03:56Kiongozi Muadhamu ametahadharisha kuhusu "maafa ya binadamu" yanayotokea Ukanda wa Gaza kwa himaya na misaada ya Marekani kwa utawala wa Israel na kubainisha kwamba, shakhsia na watu mashuhuri katika uulimwengu wa Kiislamu wanapaswa kuhimiza mwito wa kutoa pigo kali kwa utawala haramu wa Israel.
-
Ukuaji wa mara 11 ya wastani wa kimataifa wa uzalishaji sayansi nchini Iran katika kipindi cha miaka 45 iliyopita
Feb 05, 2024 23:25Katika wakati huu wa kukaribia kufanyika uchaguzi wa bunge na Baraza la Wanavyuoni Wataalamu la kumchagua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran tarehe mosi Machi, kwa mara nyingine tena maadui wa mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu wameamua kutumia vyombo vyao vya habari kujaribu kufunika na kufifiliza mafanikio ya miaka 45 ya Mapinduzi ya Kiislamuu na kuzihadaa fikra za walio wengi ili kuwafanya wananchi wasishiriki katika chaguzi hizo.
-
Mateka wa Kizayuni; mgogoro usio na kikomo kwa Benjamin Netanyahu
Feb 05, 2024 02:57Kuendelea maandamano katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ya kutaka kuachiliwa huru mateka wa Kizayuni, kumegeuka na kuwa mgogoro na jinamizi linalomkaba koo Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu pamoja na baraza lake la mawaziri.
-
Hatari za mitandao ya kijamii na juhudi za kuzitungia sheria
Feb 05, 2024 00:18Katika miaka ya hivi karibuni, mitandao ya kijamii imekuwa sehemu isiyotenganishika na maisha ya mwandamu wa sasa, kwa kadiri kwamba, ni nadra sana kumpata mtu ambaye hajajiunga kwenye mitandao hiyo na kufuatilia masuala mbalimbali anayoyapenda na yanayoivutia nafsi yake.
-
Masharti ya Muqawama wa Wapalestina ya usitishaji vita huko Gaza
Feb 04, 2024 04:14Ismail Hania, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS na Ziyad al Nakhalah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina wamefanya mazungumzo kuhusu mapendekezo ya kusimamishwa vita Gaza na kutoa masharti yao kuhusu jambo hilo.
-
Mashambulizi makubwa dhidi ya Iraq na Syria; Chokochoko mpya za Marekani eneo la Asia Magharibi
Feb 03, 2024 23:07Marekani ambayo kwa miaka kadhaa sasa imevuruga amani ya eneo la Magharibi mwa Asia kutokana na uwepo wake wa kijeshi katika eneo hilo ili kufanikisha malengo yake na ya washirika wake, imekuwa ikiyumbisha usalama wa eneo hilo nyeti na muhimu kwa kufanya mashambulizi na uvamizi wa mara kwa mara.
-
Kusambaratishwa mitandao ya kijasusi ya "Mossad" nchini Iran
Feb 03, 2024 08:32Wizara ya Intelijensia ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa imefichua vibaraka kadhaa wa shirika la ujasusi la Israel, Mossad katika nchi 28 duniani.
-
UN yaipongeza Iran kwa hatua madhubuti katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya
Feb 02, 2024 23:01Mkuu wa Idara ya Huduma za Sayansi na Maabara ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kukabiliana na Mihadarati na Uhalifu (UNODC) amepongeza hatua za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kupambana na dawa za kulevya.