-
Kufichuliwa nafasi ya jasusi wa Uholanzi katika hujumu dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran
Jan 10, 2024 02:34Gazeti la Volkskrant la Uholanzi limefichua kuwa, raia mmoja wa nchi hiyo alikuwa na mchango mkubwa katika operesheni ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuhujumu kituo cha kurutubisha uranium cha Natanz nchini Iran.
-
Indhari ya balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa kwa Marekani kuhusu vitendo vya kichochezi
Jan 09, 2024 23:12Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amekanusha madai ya Marekani na utawala wa Kizayuni katika kikao cha Baraza la Usalama kuhusu Bahari Nyekundu na kuonya dhidi ya hatua zozote za uchochezi zinazofanywa na Wamarekani.
-
Kuondoka askari wa utawala wa Kizayuni kaskazini mwa Gaza; matokeo ya kusimama kidete muqawama
Jan 09, 2024 05:29Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limethibitisha habari za kuondoka askari wake kutoka kaskazini mwa Gaza, ambapo kuondoka huko ni kukamilishwa kwa mpango wa makundi ya muqawama wa Palestina wa kulishinda jeshi vamizi.
-
Kutofautiana Baraza la Mawaziri la Israel kuhusu kutawaliwa Gaza baada ya vita
Jan 09, 2024 03:09Baraza la Mawaziri la utawala wa Kizayuni linakabiliwa na mizozo mingi, mojawapo ikiwa ni jinsi ya kuendeshwa masuala ya Gaza baada ya kumalizika vita.
-
Ombi la Italia la kuunda jeshi la Ulaya
Jan 08, 2024 22:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia, Antonio Tajani, amesema kwamba Umoja wa Ulaya unapaswa kuunda jeshi lake la pamoja ambalo linaweza kuwa na jukumu la kudumisha amani na kuzuia migogoro.
-
Kukwepa uwajibikaji na kimya cha Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa kuhusiana na jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza
Jan 08, 2024 08:41Katika kuendeleza misimamo inayozusha mizozo ya nchi za Magharibi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa amepuuza jinai zinazotekelezwa na utawala wa Kizayuni huko Gaza na kudai kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapaswa kukomesha vitendo vyake vinavyovurunga amani na uthabiti wa eneo.
-
Maandamano dhidi ya Benjamin Netanyahu ndani ya Israel na kimataifa
Jan 08, 2024 03:47Huku utawala haramu wa Israel ukiendeleza vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza maandamano dhidi ya Waziri Mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu yameenea ndani ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
Kufichuliwa pande mpya za uhusiano wa Jeffrey Epstein na wanasiasa wa Magharibi na Mossad
Jan 07, 2024 23:17Nyaraka zinazohusiana na Jeffrey Epstein, bepari na bilionea aliyepatikana na hatia ya biashara ya ngono, zimewekwa hadharani kwa amri ya jaji wa mahakama moja ya Marekani, ambapo zimeanika peupe uhusiano wa siri aliokuwa nao na watu mashuhuri wa nchi hiyo na vile vile shirika la ujasusi la utawala haramu wa Israel, Mossad.
-
Azma thabiti ya serikali ya Iraq kuondolewa nchini humo wanajeshi wa Marekani
Jan 07, 2024 04:47Waziri Mkuu wa Iraq amesisitiza katika msimamo nadra kabisa juu ya ulazima wa kuondoka nchini humo wanajeshi vamizi wa Marekani.
-
Nukta 5 za kiuchambuzi katika hotuba ya pili ya Seyyid Hassan Nasrallah mwaka 2024
Jan 07, 2024 03:59Seyyid Hassan Nasrallah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon tarehe 5 Januri katika hotuba yake ya pili katika mwaka huu mpya wa 2024 amejadili vita vya Gaza, kuuawa shahidi Saleh al-Arouri, kiongozi wa Hamas na jinai ya kigaidi huko Kerman.