-
Taathira tofauti za kusitisha mapigano na kubadilishana mateka kwa pande mbili za Israel na Palestina
Nov 30, 2023 22:57Usitishwaji vita kati ya harakati ya Hamas na utawala wa Kizayuni umerefushwa tena kwa siku moja.
-
Wito wa Umoja wa Mataifa kuhusu usitishaji vita wa kudumu huko Gaza na onyo la kuenea mapigano
Nov 30, 2023 06:13Siku ya Jumanne, ikiwa ni siku ya tano ya usitishaji vita wa muda huko Gaza, Umoja wa Mataifa ulifanya vikao viwili, kimoja katika Baraza Kuu kuhadili vita kati ya Israel na Hamas na kingine katika Baraza la Usalama kuhusu hali ya Mashariki ya Kati na Syria, ambapo vikao vyote viwili vilizungumzia kuenea mapigano katika eneo na kusisitiza juu ya udhrura wa kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu.
-
Kuharibika mfumo wa huduma za afya Ukanda wa Gaza na tishio kwa makumi ya maelfu ya watu
Nov 30, 2023 01:24Hata kama vita vimesitishwa kwa muda huko Gaza kwa kufikiwa mapatano kati ya utawala wa Kizayuni na harakati ya Hamas, lakini wasiwasi umeongezeka kuhusu hali ya huduma za afya na usafi katika ukanda huo.
-
Kuendelea siasa za chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya; kupigwa marufuku hijabu kazini
Nov 29, 2023 23:00Ikiwa ni katika muendelezo wa siasa za chuki dhidi ya Uislamu katika nchi za Magharibi, marejeo ya juu zaidi ya kushughulikia sheria za Umoja wa Ulaya imetoa uamuzi wa kupiga marufuku vazi la hijabu kwa wafanyakazi katika nchi wanachama wa umoja huo.
-
Kiongozi wa Mapinduzi asisitiza juu ya kuimarishwa utayari wa kivita wa jeshi la wanamaji.
Nov 29, 2023 08:14Akizungumza karibuni katika kikao na Kamanda Mkuu pamoja na makamanda wengine wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uwezo mkubwa wa jeshi hilo hasa katika utekelezaji wa siasa za kiuchumi baharini na kusisitiza ulazima wa kuvumbuliwa uwezo mpya kwa ajili ya kuimarisha Mfumo na taifa na vilevile kuleta matumaini na uchangamfu katika jamii.
-
Kurefushwa usitishaji vita Gaza na kuibuka changamoto mpya zinazoukabili utawala wa Kizayuni
Nov 29, 2023 04:05Usitishaji vita wa siku nne kati ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS katika Ukanda wa Gaza ulioanza saa moja asubuhi ya Ijumaa kwa saa za huko umerefushwa kwa siku mbili zaidi.
-
Nafasi muhimu ya Ansarullah katika kusitishwa vita na kuendelea kwake
Nov 28, 2023 23:13Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa serikali ya muda ya Yemen yenye mfungamano na Harakati ya Ansarullah amesema, tunakumbusha kwa mara nyingine tena kwamba, usafiri wa meli utakuwa salama kwa meli zote isipokuwa meli za utawala wa Israel katika Bahari Nyekundu.
-
Kuendelea uungaji mkono wa dunia kwa wananchi wa Palestina
Nov 28, 2023 09:39Katika muendelezo wa himaya na uungaji mkono wa ulimwengu kwa mapambano ya wananchi wa Gaza na kulaani jinai za utawala ghasibu wa Israel, maelfu ya wananchi wa Pakistan wameandamana na kuelekea katika ubalozi mdogo wa Marekani.
-
Makumi ya maelfu ya Wamorocco waandamana wakitaka kukatwa uhusiano wa nchi hiyo na Tel Aviv
Nov 28, 2023 01:45Makumi ya maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano makubwa ya kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kutaka kusitishwa juhudi za kuhuishwa uhusiano kati ya Rabat na Tel Aviv. Wafanya maandamano hao kwa mara nyingine tena wamelaani jinai za utawala haramu wa Israel na kutaka kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu huko Ukanda wa Gaza.
-
Kuongezeka upinzani dhidi ya Umoja wa Ulaya katika nchi za bara hilo
Nov 27, 2023 22:54Baada ya ushindi wa Geert Wilders, mgombea wa mrengo wa kulia wa Uholanzi katika uchaguzi wa nchi hiyo na kupendekeza kwake suala la Uholanzi kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, Marine Le Pen, kiongozi wa chama cha mrengo wa kulia cha National Rally cha Ufaransa, pia amesisitiza haya ya Ufaransa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya akisema: 'Hatupingi Ulaya, tunapinga Umoja wa Ulaya na ni kwa sababu tunaipenda Ulaya, ndio maana tunaupinga Umoja huo.'