-
Kuendelea siasa za undumakuwili za Erdogan kuhusu uungaji mkono kwa watu wa Gaza
Nov 02, 2023 08:18Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki anaendeleza siasa zake za undumakuwili katika kuunga mkono watu wa Ghaza, huku ndege za kivita za kistratijia za Marekani zikiwa zimeegeshwa katika kituo cha kijeshi cha Incirlik kusini mwa Uturuki.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: "Mauti kwa Marekani" si nara tu bali ni msimamo imara
Nov 02, 2023 04:43Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika mkutano na maelfu ya wanafunzi waliotoka katika pembe zote za Iran, ameyataja matukio ya tarehe 13 Aban 1358 (November 4, 1979) kuwa pigo la Taifa la Iran kwa Marekani.
-
Kuendelea uungaji mkono wa nchi za Magharibi kwa utawala wa Kizayuni; miaka 106 baada ya Azimio la Balfour
Nov 01, 2023 22:49Tarehe 2 Novemba 2023 inaambatana na maadhimisho ya miaka 106 ya Azimio maarufu la Balfour.
-
Ulimwengu unasubiri hatua ya kivitendo ya Mahakama ya Kimataifa kuhusu jinai za Gaza
Nov 01, 2023 08:06Katika kikao cha 21 cha mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachojadili ripoti za Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliashiria nafasi ya mahakama hiyo na kusema: Hivi sasa tunashuhudia mauaji ya kimbari yakitekelezwa katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina. Bila shaka , jinai zinazotendeka huko Ghaza ni mfano wa wazi wa jinai za kimataifa zinazopasa kushughulikiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai.
-
Wasiwasi wa viongozi wa Ulaya kuhusu kuenea barani humo uungaji mkono kwa taifa la Palestina
Nov 01, 2023 02:58Kutokana na kuendelea hujuma ya kinyama inayofanywa na utawala haramu wa Isreal katika Ukanda wa Ghaza na mauaji ya umati yanayofanywa kila siku na utawala huo dhidi ya Wapalestina hususan watoto na wanawake, mwenendo wa uungaji mkono wa kimataifa kwa kadhia ya Palestina na kulaaniwa vitendo vya jinai za Israel katika ukanda huo umeongezeka, suala ambalo limewatia wasiwasi mkubwa watawala wa Ulaya.
-
Mgawanyiko katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu; Netanyahu akiri kushindwa vyombo vya usalama na ujasusi
Oct 31, 2023 23:30Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel amefuta katika mtandao wa kijamii wa X ujumbe aliokuwa ameuandika akiashiria kushindwa vyombo vya usalama vya utawala huo kutabiri na kufuatilia shambulio la operesheni ya Kimbunga cha al- Aqsa iliyotekelezwa na wapiganaji shupavu wa Harakati ya Mapambano ya Kislamu ya Palestina Hamas.
-
Operesheni ya mauaji ya kimbari ya Israel huko Ghaza
Oct 31, 2023 05:30Katika muendelezo wa mashambulizi ya kikatili ya vikosi vya utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza, misikiti na hospitali za eneo hilo bado ni shabaha ya makusudi ya mashambulizi hayo.
-
Kuongezeka changamoto za kiuchumi kwa utawala wa Kizayuni kufuatia kuendelea vita vya Gaza
Oct 31, 2023 01:41Kimbunga cha Al Asqa na vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza vimekuwa na taathira mbalimbali ambapo moja ya taathira kuu za vita hivyo ni kuongezeka changamoto za kiuchumi kwa utawala huo.
-
Kushtadi mvutano baina ya Russia na utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 30, 2023 23:05Mvutano baina ya Russia na utawala ghasibu wa Israel umeshadidi baada ya ziara ya wawakilishi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) mjini Moscow.
-
Hatua mpya za Marekani katika fremu ya kuuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 30, 2023 08:05Tangu kuanza duru mpya ya vita kati ya utawala wa Kizayuni na makundi ya muqawama ya Palestina na operesheni ya Kimbunga ya Al-Aqsa na radiamali kali ya Wazayuni dhidi ya hatua hiyo, Marekani ikiwa mshirika wa kistratijia wa Israel imetoa himaya kubwa ya kisiasa, kidiplomasia na kijeshi kwa utawala huo ghasibu. Filihali Washington imechukua hatua mpya katika mwelekeo huu.