Mnyanyua vyuma Muirani avunja rekodi mara tatu, apata dhahabu Paralympiki Rio
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i15331
Muirani mnyanyua vyuma katika uzani wa juu zaidi amevunja rekodi tatu za dunia na kupata medali ya dhahabu katika Michezo ya Olyimpiki ya walemavu- Paralympiki-huko Rio de Janeiro, Brazil.
(last modified 2025-07-20T14:05:14+00:00 )
Sep 15, 2016 03:32 UTC
  • Mnyanyua vyuma Muirani avunja rekodi mara tatu, apata dhahabu  Paralympiki Rio

Muirani mnyanyua vyuma katika uzani wa juu zaidi amevunja rekodi tatu za dunia na kupata medali ya dhahabu katika Michezo ya Olyimpiki ya walemavu- Paralympiki-huko Rio de Janeiro, Brazil.

Katika jaribio lake la kwanza la kategoria ya kilo 107+, Siamand Rahman alinyanyua kila 270 na kuvunja rekodi ya Paralimipiki siku ya Jumatano katika ukumbi wa Riocentro.

Muirani huyo aliye na umri wa miaka 28 kisha alinyanyua kilo 300 na baadaye kilo 305 na hivyo kuvunja rekodi yake ya dunia ya kilo 296 na kwa utaratibu huo, akaipa Iran medali yake ya sita ya dhahabu katika Michezo ya Paralympiki.

Siamand Rahman akinyanyua kilo 310 katika michezo ya Paralympiki, Rio, 2016

Siamand Rahman ambaye anaiwakilisha Iran kwa mara ya pili katika Michezo ya Paralympiki, kisha aliomba kunyanya vyuma vyenye uzani wa kilo 310, baada ya kukamilisha unyanyuaji mara tatu uliohitajika katika mashindano, na hapo tena akapata mafanikio makubwa.