Meja Jenerali Salami: Adui hawezi kuvumilia kuona Iran inastawi
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i66482-meja_jenerali_salami_adui_hawezi_kuvumilia_kuona_iran_inastawi
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanahamaki na kushindwa kuvumilia hatua za maendeleo na ustawi zinazopigwa na taifa hili.
(last modified 2026-05-06T11:35:21+00:00 )
Feb 04, 2021 23:23 UTC
  • Meja Jenerali Salami: Adui hawezi kuvumilia kuona Iran inastawi

Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanahamaki na kushindwa kuvumilia hatua za maendeleo na ustawi zinazopigwa na taifa hili.

Meja Jenerali Hussein Salami aliyasema hayo jana Alkhamisi katika uzinduzi wa kituo cha nishati cha Sabalan huko Ardabil, kaskazini magharibi mwa Iran na kuongeza kuwa, adui anatiwa kiwewe na moto wa matumaini unaowaka katika nyoyo za wananchi wa Iran.

Amesema maadui wanafanya jitahada za kila aina za kutaka kuwakatisha tamaa na kuwachosha wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu.

Meja Jenerali Salami ameeleza bayana kuwa: Maadui hawalipendi taifa la Iran ambalo lina nguvu, lililostawi na kuendelea na vile vile lenye muamana, lakini wanataka kuiona Iran ambayo ni tegemezi na iliyosalimu amri.

Salami alipokitembelea kituo cha nishati cha Ardabil

Kamanda Mkuu wa jeshi la SEPAH ameongeza kuwa, wananchi wa Iran ya Kiislamu wataendelea kusimama kidete na imara kuijenga nchi yao.

Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria hatua za maendeleo zilizopigwa na Iran katika kipindi cha vikwazo na kubainisha kuwa, kuunda taifa thabiti lililostawi ni aina ya vita vinavyohitajika dhidi ya maadui na kwa msingi huo, ujenzi wa nchi hii hautasita katika wakati wowote ule.