-
Kwa nini msimamo wa Umoja wa Nchi za Kiislamu dhidi ya mpango wa "Israel Kubwa" ni hatua ya kukabiliana na kujitanua kwa utawala wa Kizayuni?
Aug 17, 2025 23:24Katika radiamali ambayo haijawahi kushuhudiwa tena huko nyuma, nchi 31 za Kiislamu zimetoa taarifa ya pamoja zikilaani mpango wa Benjamin Netanyahu wa kuunda "Israeli Kubwa" na huku zikitahadharisha kuhusu hatari ya sera hiyo ya kupenda kujitanua, zimeutaja mpango huo kuwa tishio kwa usalama wa eneo, ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na hatua ya kuchochea ghasia na ukosefu wa amani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Magaidi kadhaa waangamizwa katika operesheni ya IRGC kusini mashariki mwa Iran
Aug 17, 2025 08:48Vikosi vya usalama vya Iran vimesambaratisha mtandao mkubwa wa magaidi wakufurishaji na kuua kadhaa miongoni mwao, mbali na kunasa silaha na mabomu kadhaa katika mkoa wa kusini mashariki wa Sistan na Baluchestan.
-
Iran yamjia juu Makamu wa Rais wa ICJ kwa kuikingia kifua Israel
Aug 17, 2025 08:24Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemkosoa vikali Julia Sebutinde, Makamu wa Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kutokana na uungaji mkono wake wa wazi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Balozi wa Iran awashukuru viongozi wa serikali na kidini wa Iraq kwa kufanikisha maadhimisho ya Arbaeen
Aug 17, 2025 07:14Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Iraq ametoa shukurani zake za dhati kwa mamlaka kuu, serikali, wananchi, viongozi wa makabila na vikosi vya usalama vya Iraq kwa kuandaa kwa mafanikio maadhimisho ya Arbaeen ya Imam Hussein (as) na kulitaja suala hilo kuwa mfano usio na mbadala, wa wema na ukarimu wa Wairaki.
-
IRGC: Taifa liko tayari kuvunja safu yoyote ya adui
Aug 17, 2025 04:09Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesisitiza kuwa taifa la Iran liko tayari kusimama kidete kukabiliana na maadui wa Jamhuri ya Kiislamu na kuwalazimisha wasalimu amri kama lilivyofanya katika makabiliano yaliyopita.
-
Qalibaf: Muda wa kumdhibiti mbwa kichaa wa Kizayuni unayoyoma
Aug 15, 2025 23:27Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Gaza ndiyo "ngome ya mwisho" ya Waislamu, na kusisitiza haja ya kuungwa mkono Palestina haraka iwezekanavyo, kabla ya ardhi nyingine katika eneo kushambuliwa na kuporwa na utawala ghasibu wa Israel.
-
Kwa nini ni muhimu kuimarisha ushirikiano wa kiusalama kati ya Iran na Iraq ili kukabiliana na uingiliaji wa kigeni?
Aug 15, 2025 06:44Kuimarishwa ushirikiano wa kiusalama kati ya Iran na Iraq ni hitajio la kimkakati la kudumisha utulivu, uhuru na kukabiliana na uingiliaji wa kigeni. Ushirikiano huu sio tu kwamba unahakikisha usalama wa ndani wa nchi mbili, bali pia unaweza kuwa kielelezo cha kuunda utaratibu mpya wa kikanda unaozingatia mshikamano na muqawama.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran: Muqawama ni 'hazina kubwa' kwa eneo
Aug 15, 2025 04:01Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema, Muqawama ni "hazina kubwa" kwa eneo na Ulimwengu wa Kiislamu na akabainisha kuwa makundi ya Muqawama yamefikia kwenye "ukomavu" katika kujichukulia maamuzi yao.
-
Je, miradi ya pamoja ya mpakani kati ya Iran na Azerbaijan imeingia katika hatua mpya?
Aug 15, 2025 03:16Katika siku za hivi karibuni, sisitizo la viongozi wa Iran na Azerbaijan la kuharakisha miradi ya pamoja ya mpakani kwa mara nyingine tena limewavutia wachambuzi wa masuala ya kieneo kuhusu uhusiano wa nchi mbili hizi.
-
Human Rights Watch: Shambulio la Israel dhidi ya jela ya Evin, Iran ilikuwa jinai ya kivita
Aug 14, 2025 23:58Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limetoa ripoti na kueleza kwamba mashambulizi yaliyofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel tarehe 2 Julai dhidi ya Jela ya Evin mjini Tehran yalikuwa "kinyume cha sheria" na ni "uhalifu wa wazi wa kivita."