-
Ripoti: Starlink ilikuwa sehemu muhimu ya vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
Jun 06, 2026 04:41Ripoti mpya imefichua nafasi ya mtandao wa satalaiti wa SpaceX wa Starlink katika mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, ikisema teknolojia hiyo inayouzwa kama miundombinu ya raia imekuwa sehemu muhimu ya mashambulizi ya mauaji dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Ujumbe wa UN nchini Libya wakana kuwepo mipango ya kuwapa makazi wahamiaji nchini humo
Jun 06, 2026 04:35Ujumbe wa Msaada wa Umoja wa Mataifa nchini Libya (UNSMIL) umekana kile ulichokiita "madai" yasiyo ya kweli kuhusu kuwepo mpango wa umoja huo za kuwapa makazi wahamiaji ndani ya Libya, ukisisitiza kwamba madai haya "hayana msingi".
-
Mali yaatangaza zawadi ya dola milioni 12.4 kwa atakayesaidia kukamatwa au kuuawa viongozi wa waasi
Jun 06, 2026 04:31Serikali ya Mali imezindua kifurushi kisicho cha kawaida cha hatua za usalama, kikijumuisha zawadi kubwa za kifedha na hatua kali, kama sehemu ya kuzidisha mapambano dhidi ya makundi ya waasi yenye silaha ambayo yamezidisha mashambulizi katika miezi ya hivi karibuni, haswa baada ya shambulio la umwagaji damu la Aprili 25 lililomuua Waziri wa Ulinzi wa Mali.
-
WFP: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinasukuma mamilioni kukumbwa na njaa Afrika
Jun 06, 2026 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinawasukuma mamilioni ya watu duniani kuingia katika hali ya njaa huku bara Afrika likionekana kuathirika zaidi.
-
Utawala wa Bahrain unafuatilia malengo gani katika kuwatia mbaroni viongozi wa kidini?
Jun 05, 2026 14:06Ikiwa ni katika kuendeleza siasa zake za kuwakandamiza viongozi mashuhuri wa kidini Utawala wa Al Khalifa nchini Bahrain umewatia nguvuni viongozi wengine kadhaa wa kidini.
-
Trump sasa adai atahisi “heshima” kukutana na Kiongozi mpya wa Iran
Jun 05, 2026 11:22Rais wa Marekani Donald Trump amesema angehisi “heshima” kukutana na Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, iwapo makubaliano yatafikiwa ya kumaliza vita kati ya nchi hizo mbili.
-
Hizbullah yashambulia vikosi vamizi vya Israel kusini mwa Lebanon
Jun 05, 2026 11:19Wapiganaji wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon wametekeleza wimbi la mashambulizi yaliyoratibiwa siku ya Alhamisi, wakilenga ngome kadhaa za kijeshi za Israel na kusababisha hasara kubwa kwa wanajeshi hao vamizi wa Kizayuni.
-
Iran yaikosoa Israel na Marekani kwa kuua watoto vitani
Jun 05, 2026 11:10Iran imekosoa vikali Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuwaua watoto wasio na hatia katika nchi mbalimbali kupitia uhalifu wa kivita na uvamizi wa kijeshi.
-
Utafiti: Wamarekani waliowengi wanataka vita dhidi ya Iran visitishwe haraka
Jun 05, 2026 10:56Takribani Wamarekani saba kati ya kumi wanautaka utawala wa nchi hiyo ukomeshe vita vyake visivyo halali dhidi ya Iran “haraka iwezekanavyo.” Hayo ni kwa mujibu wa utafiti mpya uliofichua kiwango kikubwa cha kutoridhika kwa umma kuhusu mashambulizi ya kijeshi ya utawala wa Trump ambayo yanaendelea kwa zaidi ya miezi mitatu.
-
Shambulio dhidi ya timu ya mazishi ya Ebola huku maambukizi yakiongezeka DRC
Jun 05, 2026 10:53Wakazi walishambulia timu ya mazishi ya Ebola mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika jimbo la Kivu Kusini wiki hii, na kuwalazimisha wahudumu kuacha jeneza na kuzua hofu ya kuenea zaidi maambukizi ya virusi hivyo, wizara ya afya imesema.