-
Yemen yatishia kutoa jibu la pande zote kwa ongezeko lolote la mashambulizi ya Israel nchini Lebanon
Jun 03, 2026 04:10Harakati ya mapambano ya Ansarullah nchini Yemen imetangaza kuwa vikosi vya jeshi la Israel vilivyotumwa Lebanon vitaendelea kuwa katika hatari ya mashambulizi yatakayofanywa na harakati hiyo kuonyesha mshikamano na Lebanon na harakati yake ya mapambano ya Hizbullah hadi vitakapoondoka kabisa kwenye ardhi ya Lebanon.
-
Iran yazindua kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya saratani Asia Magharibi
Jun 03, 2026 04:09Iran imezindua kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya saratani katika eneo la Asia Magharibi, ambacho kinachukua nafasi ya kituo cha zamani, kwa hospitali mpya yenye ghorofa 18, vitanda zaidi ya 610 na teknolojia ya kisasa ya matibabu.
-
Shirikisho la Soka la Norway laiomba FIFA kuchunguza tuzo ya amani ya Trump
Jun 03, 2026 04:07Shirikisho la Soka la Norway (NFF) lilisema jana Jumanne kwamba limeiomba kamati ya maadili ya FIFA kuchunguza tuzo ya amani iliyotolewa na baraza linalosimamia soka duniani kwa Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Jeshi la Iran lashambulia vituo vya kijeshi vya Marekani baada ya ukiukaji karibu na Mlango wa Hormuz
Jun 03, 2026 03:01Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kwamba vikosi vyake vimetekeleza mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya meli ya adui, makao makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain, pamoja na kambi ya jeshi la anga ya Marekani katika eneo hilo, kufuatia vitendo viwili vya uchokozi wa Marekani vilivyolenga mali za Iran.
-
Wanaharakati wa haki za binadamu waandamana Nairobi kupinga kituo cha Ebola cha Marekani nchini Kenya
Jun 02, 2026 15:14Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wamefanya maandamano leo mjini Nairobi wakipinga makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali ya nchi hiyo na Marekani ya kuanzisha nchini Kenya kituo cha kuhifadhi Wamarekani wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola.
-
Lengo la Marekani kutokana na siasa zake zenye mgongano katika eneo la Asia-Pasifiki
Jun 02, 2026 10:04Waziri wa Vita wa Marekani amesema katika mkutano wa Shangri-La huko Singapore kwamba Washington inatarajia washirika wake wa Asia waongeze matumizi yao ya kijeshi na ulinzi hadi asilimia 3.5 ya Pato lao la Taifa.
-
Israel yafuta mpango wa kushambulia Beirut baada ya onyo kali la Iran
Jun 02, 2026 09:12Utawala wa Israel umeachana na mpango wake wa kufanya mashambulizi makali ya ya kijeshi dhidi ya mji mkuu wa Lebanon, Beirut. Haya yameelezwa siku ya Jumatatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia onyo kali kutoka kwa Iran kwamba haitavumilia wimbi jipya la uvamizi dhidi ya Beirut, hatua ambayo ingekiuka makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Marekani.
-
Mkuu wa Kikosi cha Quds cha IRGC aonya Bab al-Mandab itageuka kama Mlango wa Hormuz
Jun 02, 2026 09:09Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Esmail Qa’ani, ameonya kuwa Mlango wa Bab al-Mandab unaweza kukabiliwa na vikwazo vya usafiri wa meli vinavyofanana na vya Mlango wa Hormuz iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utaendelea na uhalifu nchini Lebanon na Ukanda wa Gaza chini ya himaya ya Marekani.
-
Waliowengi Baraza la Usalama la UN walaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon
Jun 02, 2026 09:08Idadi kubwa ya wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wameonyesha kutokuridhishwa kwao na kuongezeka kwa mashambulizi ya kijeshi ya Israel dhidi ya Lebanon. Wakati hayo yakijiri, Marekani imepuuza kuukosoa utawala wa Israel, badala yake ikielekeza lawama zake zote kwa harakati ya Muqawama ya Hizbullah na nchi ya Iran.
-
Visa vya Ebola vimefika 300 nchini DR Congo huku maeneo zaidi ya afya yakiathirika
Jun 02, 2026 09:06Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imevuka 300 kufikia Jumatatu.