-
Raia watano wa Msumbiji wauawa katika ‘Mashambulizi ya Chuki’ nchini Afrika Kusini
Jun 02, 2026 09:01Serikali ya Msumbiji imetangaza kuwa takriban raia wake watano wameuawa katika “mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni” nchini Afrika Kusini mwishoni mwa juma lililopita. Vifo hivyo vinaashiria kushadidia maandamano yanayoendelea nchi nzima dhidi ya wahamiaji wasio na vibali.
-
Qalibaf: Marekani ni lazima ilipe gharama za jinai za Israel Lebanon
Jun 02, 2026 03:01Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) Mohammad Baqir Qalibaf ameilaani Marekani kwa kuhusika katika mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Lebanon na kueleza kuwa Washington lazima ilipe gharama ya jinai za kivita zinazofanywa na utawala huo ghasibu dhidi ya Lebanon.
-
IRGC yapiga kambi ya anga ya Marekani iliyohusishwa na shambulio dhidi ya mnara wa mawasiliano kusini mwa Iran
Jun 02, 2026 02:59Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema limefanya shambulio la kulipiza kisasi dhidi ya kambi ya anga iliyotumiwa na Marekani kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya mnara wa mawasiliano katika kusini mwa Iran.
-
Bei ya mafuta duniani yapanda huku majeshi ya Israel yakisonga ndani zaidi kusini mwa Lebanon
Jun 02, 2026 02:56Bei ya mafuta duniani yapanda huku majeshi ya Israel yakisonga ndani zaidi kusini mwa Lebanon
-
Walimu Nigeria waitisha mgomo katika jimbo la Oyo kufuatia vitendo vya utekaji nyara shuleni
Jun 02, 2026 02:53Muungano wa Walimu wa Nigeria umeitisha mgomo wa wazi kuanzia leo Jumatatu katika jimbo la Oyo kupinga kutekwa nyara makumi ya watoto na walimu wao katikati ya mwezi wa Mei mwaka huu.
-
Jeshi la Somalia lamuuwa kamanda mwandamizi wa kundi la kigaidi la Al Shabaab
Jun 02, 2026 02:51Jeshi la Taifa la Somalia (SNA) limewaua wanachama wawili wa kundi la kigaidi la Al Shabaab, akiwemo kamanda mwandamizi, katika operesheni ya kijeshi iliyopangwa katika eneo la Hanti Wadaag, mkoani Lower Shabelle.
-
Rais Ruto aagiza ujumuishaji wa Shule za Kiislamu katika mfumo rasmi wa elimu wa Kenya
Jun 01, 2026 13:06Rais wa Kenya, William Ruto, amemwagiza waziri wa elimu kushirikisha wadau wote husika na kuanzisha mashauriano kuhusu ujumuishaji rasmi wa shule za Kiislamu nchini, zinazojulikana kama Duksi au Madrasa, katika mfumo wa elimu wa Kenya.
-
Wanawake wako katika hatari kubwa ya kuathiriwa na mlipuko wa Ebola Kongo
Jun 01, 2026 11:44Wakati Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikiendelea na mapambano dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola, wanawake nchini humo wametajwa kuwa kundi lililo kwenye hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo unaosababishwa na virusi.
-
Watu 12 wauawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya Israel katika ardhi ya Lebanon
Jun 01, 2026 11:24Ikiwa ni katika muendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya usitishaji vita na mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya miji na vijiji vya kusini mwa Lebanon yaliyotekelezwa zaidi ya mara 36 mchana na Jumapili usiku, watu 12 wameuawa shahidi na wengine 35 kujeruhiwa katika mashambulizi hayo ya jinai.
-
Kauli ya Umoja wa Ulaya inayolaani kujilinda halali kwa Iran ni ya kinafiki
Jun 01, 2026 11:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa Umoja wa Ulaya unapasa kuzingatia kanuni ya utawala wa sheria na Hati ya Umoja wa Mataifa ambazo unadai kufungamana nazo.