-
Je, ni vipi Ulaya imekuwa mshirika wa jinai za utawala wa Kizayuni?
Jun 01, 2026 09:59Jürgen Todenhofer, mwanasiasa na mjumbe wa zamani wa bunge la Ujerumani, amesema: "Umoja wa Ulaya na serikali ya Ujerumani zinahusika moja kwa moja katika maangamizi makubwa ya watu wa Palestina."
-
Yemen: Kupiga marufuku Hamas na Jihad Islami kunaonyesha jinsi Ulaya inavyoukingia kifua Uzayuni wa kimataifa.
Jun 01, 2026 09:24Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imelaani vikali hatua ya Umoja wa Ulaya ya kuimarisha vikwazo dhidi ya harakati za ukombozi wa Palestina, Hamas na Jihad Islami, ikiitaja kuwa ni ishara ya utiifu kwa Uzayuni wa kimataifa.
-
Iran yalaani vikali shambulio la polisi wa Uholanzi dhidi ya mke mjamzito wa Mpalestina
Jun 01, 2026 09:13Iran imelaani vikali shambulio la kikatili lililofanywa na polisi wa Uholanzi dhidi ya mke mjamzito wa mwanamume Mpalestina, ikitoa wito kwa serikali ya Uholanzi kuchunguza tukio hilo na kuwawajibisha waliohusika.
-
Spika Qalibaf: Iran inamrudisha nyuma adui kupitia umoja wa kitaifa
Jun 01, 2026 03:24Mohammad Baqir Qalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa Iran, kupitia umoja wa kitaifa, inamrudisha nyuma adui katika vita vinavyoacha historia.
-
Mwanasiasa wa Ujerumani: EU ni mshirika katika ugaidi wa kimfumo wa Israel
Jun 01, 2026 02:55Mwanasiasa wa Ujerumani na mbunge wa zamani wa bunge la nchi hiyo amekosoa sera za utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema: "Walowezi wa Kizayuni wanafanya ugaidi wa kimfumo dhidi ya Wapalestina, na serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya wanashiriki katika uhalifu huo kwa kunyamaza kimya."
-
WHO: Uvutaji sigara unahatarisha afya ya watu bilioni 1.2 duniani kote
Jun 01, 2026 02:47Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza takwimu za kutisha na za kusikitisha kuhusu hatari ya uvutaji sigara, kwa mnasaba wa madhimisho ya kila mwaka ya Siku ya Kupiga Vita Tumbaku Duniani, ambayo huadhimishwa Mei 31.
-
Uchaguzi mkuu Ethiopia; Abiy Ahmed anatarajiwa kushinda tena kiti cha Waziri Mkuu
Jun 01, 2026 02:42Uchaguzi mkuu wa Ethiopia unatarajiwa kufanyika Jumatatu hii huku migogoro ikiendelea katika baadhi ya maeneo ya nchi, ikimaanisha kuwa watu wengi hawataweza kupiga kura.
-
Mkaguzi mkuu wa magereza Ufaransa: Hali ya magereza nchini ni "mbaya, ya aibu na ya majanga"
Jun 01, 2026 02:39Wizara ya Sheria ya Ufaransa imetangaza kwamba idadi ya wafungwa nchini humo imefikia zaidi ya watu 88,600, ambayo ni kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa katika historia ya nchi hiyo.
-
Kwa nini Trump anatapatapa kati ya vitisho na makubaliano?
May 31, 2026 13:18CNN imesema katika ripoti kwamba: "Serikali ya Marekani huchanganyikiwa linapokuja suala la nyuklia la Iran." Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita, Rais Donald Trump wa Marekani amebadilisha misimamo yake mara kadhaa kuhusu hatima ya hifadhi ya urani iliyorutubishwa ya Iran.
-
Trump anakabiliwa na chaguzi 'mbaya' au 'mbaya zaidi' kuhusu Iran: Jenerali wa IRGC
May 31, 2026 12:56Kamanda wa cheo cha juu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) anasema Rais wa Marekani, Donald Trump, hana chaguo zuri kuhusu Iran na anapaswa kuchagua kati ya njia "mbaya" au "mbaya zaidi".