-
Msemaji wa serikali ya Afghanistan: Tutaiunga mkono Iran kama itakabiliwa na uadui
Feb 16, 2026 02:25Msemaji wa serikali ya Afghanistan amesisitiza kwamba watu wa Afghanistan wataonyesha mshikamano na kutoa aina mbalimbali za misaada kwa Iran iwapo kutatokea uchokozi wowote dhidi ya nchi hiyo.
-
Je, China ina msimamo gani kuhusu hatua mpya za utawala wa Israel katika Ukingo wa Magharibi?
Feb 16, 2026 00:05China sambamba na kuashiria kuidhinishwa kanuni mpya na baraza la mawaziri la usalama la Israel ili kuimarisha udhibiti wa Ukingo wa Magharibi, imeonya kuhusu matokeo mabaya ya hatua hiyo.
-
Jenerali Mousavi: Mapambano dhidi ya Iran yatakuwa funzo kwa Trump
Feb 16, 2026 00:02Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Donald Trump anapaswa kufahamu kwamba kuingia katika mapambano ya kijeshi na Iran kutakuwa funzo lenye athari kubwa, ambalo matokeo yake yatamzuia kufanya vitisho na majigambo kwenye jukwaa la kimataifa.
-
Palestina yataka uingiliaji kati wa walimwengu kusitisha mashambulizi ya Israel
Feb 16, 2026 00:01Mamlaka ya Ndani ya Palestina, imetoa radiamali kwa uamuzi wa baraza la mawaziri la utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kutaifisha ardhi za Ukingo wa Magharibi na kuitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua kuhusu suala hilo.
-
Iran yaingia kwenye klabu ya mataifa yenye bidhaa za juu za tiba ya seli
Feb 15, 2026 23:29Taasisi ya Utafiti ya Royan Research ya Iran imezindua bidhaa sita mpya zilizotengenezwa ndani ya nchi katika nyanja ya tiba ya seli na uhandisi wa tishu, hatua inayoiweka Iran miongoni mwa mataifa yanayozalisha bidhaa za kisasa za tiba zinazojulikana kama Advanced Therapy Medicinal Products (ATMPs).
-
Umoja wa Afrika wapitisha “Azimio la Algiers” kuhusu uhalifu wa kikoloni barani Afrika
Feb 15, 2026 23:28Kikao cha 39 cha kawaida cha Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kilichofanyika Jumapili jijini Addis Ababa kimepitisha “Azimio la Algiers” kuhusu uhalifu wa kikoloni barani Afrika, huku pia kikiidhinisha tarehe 30 Novemba kuwa Siku ya Afrika ya Mashahidi wa Bara Afrika
-
Wapalestina 10 wauawa katika mashambulizi ya Israel Gaza licha ya usitishaji vita
Feb 15, 2026 23:27Vikosi vya Israel vimewaua angalau Wapalestina 10 katika mashambulizi mapya yaliyofanywa katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji mwingine wa makubaliano ya usitishaji vita yaliyoratibiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa Oktoba 10 mwaka jana.
-
Sheikh Maher Hammoud: Uvamizi wa kijeshi dhidi ya Iran utawasha moto Asia Magharibi
Feb 15, 2026 08:47Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Muqawama amesema kuwa, uchokozi wowote mpya dhidi ya Iran utapelekea kuwaka moto katika eneo lote la Asia Magharibi.
-
Mvutano waongezeka kati ya Netanyahu na Herzog baada ya Trump kumtusi Rais wa Israel
Feb 15, 2026 08:03Hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kumtusi Rais wa utawala wa kizayuni wa Israel akimuunga mkono waziri mkuu wa utawala huo yameongeza mvutano kati ya Netanyahu na Isaac Herzog.
-
Katibu Mkuu wa Hizbollah: Iran daima imekuwa ikiunga mkono Palestina na wanyonge duniani
Feb 15, 2026 07:29Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbollah ya Lebanon amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa ikiunga mkono Palestina na watu wanaokandamizwa duniani.