-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Iran: Mpira uko kwenye uwanja wa Marekani kuthibitisha azma ya kufikia makubaliano ya nyuklia
Feb 15, 2026 07:26Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema ni zamu ya Marekani kuonyesha azma ya kufikia makubaliano yanayolenga kutatua suala la nyuklia la Tehran.
-
"Hatuui tu, tunabaka": Mwanajeshi wa Israel aliyeua watu Gaza akiri kufanya uhalifu
Feb 15, 2026 06:54Mwanajeshi mmoja katika jeshi la Israel ametoa kauli ya kushtua katika mahojiaano ya moja kwa moja na YouTuber wa Marekani, akizungumzia vitendo vinavyofanywa na wanajeshi wa utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza katika vita vya mauaji ya kimbari.
-
Kutoka Kongamano la Usalama hadi "Sarakasi ya Munich"; Msimamo wa Iran Kuhusu Matukio ya Ulaya
Feb 15, 2026 04:48Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa: Ni jambo la kusikitisha kuona kwamba Kongamano la Usalama la Munich ambalo kwa kawaida huzingatiwa kuwa tukio muhimu na lenye hadhi kubwa, limegeuka kuwa "sarakasi ya Munich" kuhusu masuala ya Iran.
-
Araqchi: Sarakasi ya Munich dhidi ya Iran imedhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki
Feb 15, 2026 04:30Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Mkutano wa Usalama wa Munich uliokua na mtazamo dhidi ya Iran umegeuka na kuwa kongamano la sakarakasi na hivyo kudhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki na umuhimu wa kistratejia.
-
Baqaei: Mashinikizo ya kisiasa hayawezi kudhoofisha haki ya Iran ya kurutubisha urani
Feb 15, 2026 04:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa haki "isiyoweza kubatilishwa" ya Iran ya kurutubisha madini ya urani haiwezi kudhoofishwa na mashinikizo ya kisiasa.
-
Waasi wenye silaha wauwa watu wasiopungua 32 kaskazini mwa Nigeria
Feb 15, 2026 04:28Watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki wamevamia vijiji vitatu kaskazini mwa Nigeria, na kuua takriban watu 32 na kuwateka nyara wengine kadhaa.
-
Madagascar yatangaza kimbunga Gezani janga la kitaifa
Feb 15, 2026 04:27Serikali ya Madagascar jana ilitangaza kuwa kimbunga cha Gezani kilichoiathiri nchi hiyo ni janga la kitaifa. Kimbunga hicho cha kitropiki kmesasabisha vifo vya watu 43, majeruhi kadhaa, uharibifu wa miundombinu na makazi na hasara kubwa katika baadhi ya maeneo.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia ahimiza kuwepo uhusiano wa heshima kati ya Afrika na Italia
Feb 15, 2026 04:26Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia amehimiza kuhusu ushirikiano mpya kati ya Afrika na Ulaya unaozingatia utu na ustawi wa pamoja. Waziri Mkuu wa Ethiopia ameeleza haya alipokuwa mwenyeji wa Mkutano wa Pili wa Italia na Afrika mjini Addis Ababa mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Rais Pezeshkian: Nchi za eneo zinaweza kutatua matatizo yao bila kusimamiwa
Feb 14, 2026 23:57Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba kuanzisha amani na utulivu ndiyo "njia ya maisha kwa sayari hii ndogo," akisisitiza kuwa nchi za eneo zinaweza kutatua matatizo yao bila kusimamiwa na kwamba, hakuna nchi itakayofaidika na vita, migogoro, vurugu, na umwagaji damu.
-
Israel yakasirishwa na kauli ya kumdhalilisha rais wake iliyotolewa na Trump
Feb 14, 2026 23:56Duru zilizo karibu na rais wa utawala wa kizayuni wa Israel zimeyaelezea matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kumtusi na kumdhalilisha rais wa utawala huo Isaac Herzog kuwa ni uvukaji mistari myekundu.