-
Umoja wa Afrika: Mateso dhidi ya Wapalestina lazima yakomeshwe
Feb 14, 2026 23:20Mahmoud Ali Youssouf Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) amesema kuwa, mauaji dhidi ya wananchi wa Palestina ni lazima yakomeshwe. Mahmoud Ali Youssouf alisema hayo jana (Jumamosi) wakati akiufungua mkutano wa kilele wa 39 wa umoja huo.
-
China: Tofauti kati ya Iran na Marekani zinapaswa kutatuliwa kupitia mazungumzo
Feb 14, 2026 23:19Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa China amesisitiza kuwa, tofauti kati ya Iran na Marekani zinapaswa kutatuliwa kupitia mazungumzo na upatanishi, na akaonya kwamba mvutano kati ya nchi hizo mbili unaweza kuathiri moja kwa moja amani na utulivu katika Asia Magharibi.
-
Mbunge wa Kongresi: Marekani iliwezesha mauaji ya halaiki Ukanda wa Gaza
Feb 14, 2026 23:19Mbunge wa chama cha Democratic katika Kongresi ya Marekani amesema kuwa, msaada wa kijeshi wa Marekani kwa Israel "usio na masharti" uliwezesha mauaji ya halaiki huko Gaza," akibainisha kuwa maelfu ya wanawake na watoto waliuawa katika matukio ambayo "yangeweza kuepukwa kabisa."
-
Ubepari na ukosefu wa utulivu wa kijamii
Feb 14, 2026 23:18Uhusiano kati ya ubepari na ukosefu wa utulivu wa kijamii ni mojawapo ya mada muhimu katika uwanja wa sayansi za jamii.
-
Je dunia kweli imekubali uongozi wa Marekani?
Feb 14, 2026 07:12Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa amedai dunia imekaribisha nafasi ya uongozi wa Marekani.
-
Reuters: Duru ya pili ya mazungumzo ya Iran na Marekani itafanyika Jumanne, Geneva
Feb 14, 2026 06:26Shirika la habari la Reuters limenukuu chanzo kimoja na kutangaza kuwa ujumbe wa Marekani unaojumuisha Steve Witkoff na Jared Kushner, utakutana na maafisa wa Iran mjini Geneva, Uswisi siku ya Jumanne wiki hii.
-
Ripota maalumu wa UN: Hujuma dhidi yangu si chochote kulinganisha na mateso ya Wapalestina
Feb 14, 2026 06:26Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu amesema, analengwa na hujuma za kumchafulia jina na kumtaja kwa ubaya kwa sababu ya kulaani vita vya utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza na Ukingo wa Magharibi.
-
Katibu Mkuu wa UN: Lazima Afrika iwe na sauti na iweze kunufaika na rasilimali zake
Feb 14, 2026 06:26Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito mkali wa kuhakikisha haki na mageuzi yanatekelezwa na kuimarishwa ushirikiano wa kimataifa, huku akiutaja Umoja wa Afrika AU, kama “kinara wa ushirikiano wa kimataifa katika dunia iliyogawanyika”.
-
BNP kutangaza serikali mpya ya Bangladesh Jumapili, kuitaka India imrudishe Hasina
Feb 14, 2026 06:25Chama cha Taifa cha Bangladesh (BNP) kimetangaza kuwa kitaunda serikali mpya ifikapo kesho Jumapili, baada ya kupata ushindi wa kishindo wa theluthi mbili ya viti vya Bunge katika uchaguzi wa kwanza kufanyika nchini humo tangu mapinduzi ya Julai 2024 yaliyoing'oa madarakani serikali ya aliyekuwa waziri mkuu Sheikh Hasina.
-
Rais Xi Jinping wa China: Tutaziondolea ushuru nchi za Afrika ifikapo mwezi Mei
Feb 14, 2026 06:25Rais Xi Jinping wa China ametangaza kuwa, nchi yake itaziondolea ushuru nchi zingine za Afrika ifikapo mwezi Mei mwaka huu.