-
Walinzi wa mpaka wa Iran na Iraq washirikiana kuandaa marasimu ya Arbaeen
Jun 19, 2026 12:35Walinzi wa mpaka wa pamoja wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Jamhuri ya Iraq wamefanya vikao vya pamoja katika mpaka wa eneo la Mehran katika mkesha wa kuanza rasmi wimbi kubwa la mazuwwar wa Muharram na Arbaeen.
-
Imam wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran: Utawala wa Marekani hauaminiki hata kidogo
Jun 19, 2026 12:27Huku akisema kuwa, nguvu ni matunda ya subira mitaani, medani ya vita na diplomasia kwa pamoja, Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya mjini Tehran amesisitiza kuwa: 'Leo utawala wa Marekani hauaminiki hata kidogo.'
-
Mkataba wa Maelewano na Iran: Mwisho wa nguvu ya Dola la Marekani
Jun 19, 2026 12:25Tucker Carlson, mtangazaji na mchambuzi mashuhuri wa Marekani, amesema katika taarifa kuhusu makubaliano ya hivi karibuni kati ya Iran na Marekani kwamba makubaliano hayo yamemaliza kikamilifu nguvu, kiburi, majigambo na ubabe wa Marekani katika ngazi ya kimataifa na kuipelekea ikiri rasmi hadharani kwamba Iran ni mchezaji muhimu mwenye maamuzi huru, na kwamba hilo pekee limebadilisha kila kitu katika mtazamo wa kisiasa na kijeshi.
-
Utawala wa Kizayuni wakiri kuuawa na kujeruhiwa wanajeshi wake 22 katika mapigano ya kusini mwa Lebanon
Jun 19, 2026 12:24Jeshi la utawala wa Kizayuni limetangaza kuuawa na kujeruhiwa askari wake 22 katika mapigano ya jana Alhamisi jioni na vikosi vya muqawama vya Hizbullah ya Lebanon.
-
Iran yalaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya misikiti ya Ukingo wa Magharibi
Jun 19, 2026 12:20Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vitendo vya Wazayuni kuvunjia heshima na kushambulia misikiti ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Kutoka uwanja wa vita hadi meza ya mazungumzo; Je, Iran imebadilisha vipi milinganyo ya vita?
Jun 19, 2026 10:27Kusainiwa Mkataba wa Maelewano wa Islamabad na Marais wa Iran na Marekani kunashiria mwisho wa mojawapo ya mivutano na makabiliano makubwa zaidi kati ya nchi hizi mbili.
-
Kiongozi Muadhamu apongeza juhudi za maafisa wa Iran, asema Trump alitamani sana kufikia makubaliano
Jun 19, 2026 04:02Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema maafisa wa Iran wamefanya juhudi kubwa kwa nia njema kufikia makubaliano ya maelewano na Marekani, huku rais wa Marekani akitumia njia mbalimbali za mashinikizo kutokana na kukata tamaa.
-
Rais Pezeshkian apongeza hati ya makualiano na Marekani; asema ni ushahidi wa 'Iran yenye nguvu'
Jun 19, 2026 03:59Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesifu hati ya makubaliano ya Islamabad iliyotiwa saini kati ya Iran na Marekani kuwa ni "hati ya kihistoria" na dhihirisho la nguvu ya Iran duniani.
-
Jihad Islami yailaumu Marekani kwa ukatili unaoendelezwa na Israel huko Gaza
Jun 19, 2026 03:50Harakati ya Jihadi Islami ya Palestina imesema utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani lazima uwajibishwe kwa ukatili na vitendo vya uchokozi vinavyofanywa na askari wa utawala vamizi wa Israel dhidi ya Wapalestina wa kawaida katika Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita.
-
Wanasayansi: Aina ya sasa ya Ebola imeitoka kwa wanyamapori
Jun 19, 2026 03:46Ugonjwa wa sasa wa Ebola, ambao ulizuka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda mwezi uliopita, ni matokeo ya kuenea kwa wanyamapori. Haya yameelezwa na wanasayansi kutoka nchi hizo mbili jana Alhamisi.