-
Kimbunga Gezani chaikumba Madagascar, chaua 20 na kujeruhi 33
Feb 11, 2026 22:59Kimbunga cha Tropiki cha Gezani kimepiga mji wa bandari wa Toamasina ulioko kwenye pwani ya mashariki mwa Madagascar, na kuua watu wasiopungua 20 na kujeruhi wengine 33 katika jiji hilo la pili kwa ukubwa kwenye kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi, huku mvua kali na upepo vikisababisha uharibifu mkubwa. Hayo ni kwa mujibu wa mamlaka husika ya nchi hiyo.
-
Kashfa ya Epstein ilivyofichua mmomonyoko wa kimaadili katika nchi za Magharibi
Feb 11, 2026 22:59Wimbi la kujiuzulu linaloshuhudiwa huko Downing Street, kuanzia mkuu wa wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza hadi mkurugenzi wake wa mawasiliano, ni ishara za nje za mgogoro mkubwa wa kimaadili miongoni mwa wasomi na viongozi wa Magharibi.
-
Azimio la maandamano ya Bahman 22: Tunaunga mkono kwa 100% diplomasia na medani ya kijeshi
Feb 11, 2026 10:30Wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran waliohudhuria maandamano ya Bahman 22 mjini Tehran wameidhinisha azimio la maandamano hayo na kutangaza kwamba, sasa ni wakati wa ushirikiano kati ya medani ya kijeshi na ya diplomasia, na kwamba askari wa nyuga zote hizo mbili wanatokana na kizazi cha taifa na wanaungwa mkono kwa asilimia mia moja na wananchi wa Iran.
-
Kengele ya hatari ya Russia kuhusu matokeo mabaya ya chokochoko yoyote dhidi ya Iran
Feb 11, 2026 06:59Serikali ya Russia imeonya kuhusu matokeo mabaya ya kuanzisha chokochoko yoyote dhidi ya Iran.
-
Mkuu wa Jumuiya ya Madola ahimiza kasi kuelekea mazungumzo ya fidia ya utumwa
Feb 11, 2026 06:18Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth), kundi la mataifa 56 linaloongozwa na Mfalme Charles wa Uingereza, amesema anatarajia nchi wanachama wa jumuiya hiyo zitapiga hatua ya kuanza mazungumzo kuhusu fidia ya biashara ya utumwa iliyovuka Bahari ya Atlantiki.
-
Hamas: Ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu mateka inathibitisha uhalifu wa Israel
Feb 11, 2026 06:02Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kwamba taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa, ambayo imerekodi ukatili unaofanywa na utawala vamizi wa Israel dhidi ya mateka wa Kipalestina katika vituo na mahabusi zake, inathibitisha zaidi ukiukaji wa sheria za kimataifa ambao haujawahi kutokea unaofanywa na utawala huo.
-
Rais wa Colombia asema amenusurika jaribio la mauaji
Feb 11, 2026 06:02Rais Gustavo Petro wa Colombia amesema alinusurika jaribio la mauaji jana Jumanne, baada ya miezi kadhaa ya maonyo kuhusu njama inayomlenga ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya.
-
Pezeshkian: Dunia ishuhudie jinsi Wairani walivyojitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya Bahman 22 ili kuihami nchi yao
Feb 11, 2026 06:00Rais Masoud Pezeshkian amesema kuwa dunia inapasa kuona jinsi mailioni ya wananchi wa Iran walivyomiminika mitaani katika maandamano ya mamilioni ya wananchi kote nchini ili kulinda mapinduzi yao, kutii uongozi wa mfumo, na kutetea thamani na nchi yao ya kujivunia.
-
Mamilioni wamiminika mitaani Iran kuadhimisha ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Feb 11, 2026 03:38Mamilioni ya wananchi kutoka matabaka yote ya kijamii wamejitokeza mitaani kote nchini Iran kushiriki maandamano ya kitaifa yanayoashiria maadhimisho ya miaka 47 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Serikali ya Kenya kusaidia familia za Waislamu wenye njaa mwezi wa Ramadhani
Feb 11, 2026 03:35Serikali ya Kenya imeweka mpango wa kusaidia familia za Kiislamu zilizo katika mazingira magumu huku zikijiandaa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhan wiki ijayo.