Nov 30, 2020 13:14
Baada ya makundi ya kigaidi kudhoofishwa katika maeneo mbali mbali ya Asia Magharibi, hivi sasa makundi hayo yameeneza satwa yao na kuimarika katika maeneo mbali ya barani Afrika ambapo yamekithirisha hujuma. Katika tukio la hivi karibuni, magaidi wakufurishaji wa Boko Haram wameua wakulima 110 katika kijiji cha Koshobe karibu na Maiduguri, mji mkuu wa jimbo la Borno ambalo ni kitovu cha magaidi hao, kaskazini mashariki mwa Nigeria.