-
Syria: Magaidi wanazuia raia kutoka mji wa Aleppo
Oct 21, 2016 10:23Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesema wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wanawazuia raia kuugura mji wa Aleppo, ambao kwa sasa unashuhudia makabiliano makali kati ya vikosi vya serikali na magenge ya kigaidi.
-
Mufti wa Syria awataka magaidi kujisalimisha huko Aleppo
Oct 21, 2016 01:12Mufti wa Syria amewataka magaidi walioko nchini humo kujisalimisha wenyewe kabla ya kuanza operesheni kubwa na ya pande zote ya jeshi la nchi hiyo ya kukomboa kikamilifu maeneo yote ya mji huo.
-
Jeshi la Libya lasonga mbele Sirte, magaidi wa Daesh waendelea kupigwa
Oct 21, 2016 00:29Jeshi la Libya linaloiunga mkono serikali ya umoja wa kitaifa limesonga mbele zaidi katika mji wa Sirte unaotambuliwa kuwa ngome kuu ya kundi la kigaidi la Daesh nchini humo.
-
Russia yaionya Marekani dhidi ya kuwatoa magaidi Iraq hadi Syria
Oct 20, 2016 00:34Russia imeionya Marekani dhidi ya kuwafurusha wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh kutoka Iraq hadi Syria, katika mashambulizi yake ya kuukomboa mji wa Mosul, kaskazini mwa Iraq.
-
Iraq: Nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi, wafadhili wa Daesh
Oct 18, 2016 03:38Waziri Mkuu wa Iraq amesema nchi kadhaa za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi zinaliunga mkono na kulifadhili kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, linalofanya jinai za kutisha nchini humo na Syria.
-
Marekani, Saudia, Israel ni waungaji mkono wa magaidi wa Daesh
Oct 17, 2016 23:40Kamanda wa ngazi za juu wa jeshi nchini Syria amesema, kuna ushahidi wa kutosha kuwa Marekani, Saudi Arabia na Israel ni waungaji mkono wakuu wa magaidi wa ISIS (Daesh) huko Syria na Iraq.
-
Magaidi zaidi waangamizwa katika mkoa wa Salahuddin nchini Iraq
Oct 17, 2016 12:23Jeshi la Iraq limetangaza habari ya kushadidisha mashambulizi yake katika mkoa wa Salahuddin wa kaskazini mwa Baghdad, mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Mgogoro wa kisiasa waongezeka nchini Libya
Oct 17, 2016 12:20Taasisi ya kulinda usalama iliyoko chini ya amri ya baraza la uongozi wa Libya imetangaza kujitenga na baraza hilo.
-
Mufti wa Misri awaambia Wamagharibi: Daesh si "Dola la Kiislamu"
Oct 06, 2016 12:17Mufti wa Misri amevitaka vyombo vya habari vya nchi za Magharibi viache kutumia neno "Dola la Kiislamu" kuliarifisha kundi la kigaidi la Daesh.
-
Mkuu wa Daesh taabani baada ya kupewa sumu
Oct 05, 2016 11:23Mkuu wa kundi la kigiaid la ISIS (Daesh), Ibrahim al-Samarrai, maarufu kama Abu Bakr al-Bahgdadi, ameripotiwa kuwa katika hali mbaya ya kiafya baada ya kuwekewa sumu katika chakula chake.