-
Bunge la Libya lapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya umoja wa kitaifa
Aug 23, 2016 08:12Wabunge wa Libya wamepiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya umoja wa kitaifa inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.
-
Serikali ya Libya yapigiwa kura ya kutokuwa na imani nayo
Aug 22, 2016 23:40Serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imepata pigo kubwa baada ya wabunge katika bunge la nchi hiyo linalotambuliwa kimataifa kuikataa.
-
Jeshi la Libya: Tumekomboa msikiti na jela Sirte kutoka mikononi mwa Daesh
Aug 22, 2016 11:35Vikosi vya jeshi Libya vimetangaza kuwa vimeukomboa msikiti mkuu wa mji wa Sirte na jela ya mji huo kutoka mikononi mwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, katika operesheni ya kulitimua kundi hilo la kigaidi katika mji huo ulioko kwenye pwani ya kusini ya Ghuba ya Sidra.
-
Wanajeshi kadhaa wauawa kaskazini mashariki mwa Libya
Aug 21, 2016 23:28Vyombo vya habari vya nchi za Kiarabu vimeripoti habari ya kuuawa wanajeshi kadhaa wa Jenerali Khalifa Haftar katika mripuko wa bomu uliotokea kaskazini mashariki mwa Libya.
-
Zaidi ya watu 38 wauawa mashariki mwa Libya
Aug 16, 2016 23:27Baraza la Shura ya Wanamapinduzi la Benghazi limetangaza kuwa wapiganaji 38 watiifu kwa Jenerali Khalifa Haftar wameuawa katika mapigano na vikosi vitiifu kwa baraza hilo huko Benghazi mashariki mwa Libya.
-
42 wauawa na kujeruhiwa katika shambulizi la bomu Libya
Aug 02, 2016 23:27Makumi ya watu wameuawa na kujeruhiwa katika shambulizi la bomu la kutegwa garini lililolenga wanajeshi wa serikali katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya.
-
Ghala la silaha za Daesh lanaswa Sirte, Libya
Jul 31, 2016 11:49Vikosi vya jeshi la Libya vimegundua na kunasa karakana moja ya kuzalisha mabomu ya kutega ardhini, mada za miripuko na ghala lililokuwa na silaha za aina mbalimbali mali ya kundi la kigaidi la Daesh huko mashariki mwa mji wa Sirte nchini humo.
-
Askri kadhaa wa Libya wauawa katika mapigano mapya Sirte
Jul 30, 2016 03:33Mapigano mapya baina ya askari wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya na genge la kigaidi la Daesh yamesababisha mauaji ya askari watano wa serikali katika mji wa Sirte, kaskazini mwa nchi hiyo.
-
UN yapitisha muswada wa kuangamizwa silaha za kemikali za Libya
Jul 23, 2016 08:37Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja muswada wa kuhamishia silaha za kemikali za Libya nje ya nchi hiyo kwa ajili ya kuharibiwa.
-
Matamshi ya afisa jeshi wa Libya kuhusu kuweko nchini vikosi ajinabi
Jul 23, 2016 02:32Kamanda wa kikosi cha anga cha jeshi la Libya amesema kuwa wanajeshi wa Marekani, Uingereza na Ufaransa wapo Libya kwa ajili tu ya kudhibiti harakati za kundi la kigaidi la Daesh.