-
Bunge la Uturuki laidhinisha kutumwa askari wa nchi hiyo Libya
Jan 02, 2020 23:23Bunge la Uturuki limepasisha muswada wa sheria inayoruhusu kutumwa wanajeshi wa nchi hiyo huko Libya.
-
Uturuki: Hatutapeleka askari Libya ikiwa vikosi vya Haftar vitasitisha mashambulio dhidi ya Tripoli
Jan 02, 2020 00:23Makamu wa Rais wa Uturuki Fuat Oktay amesema, nchi yake haitapeleka askari Libya ikiwa vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar vitasitisha mashambulio dhidi ya mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Arab League yaonya juu ya kutumwa majeshi ajinabi Libya
Jan 01, 2020 04:30Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imeziasa pande hasimu za kisiasa nchini Libya kujiepusha na hatua yoyote ambayo itachochea kutumwa vikosi vya nchi za kigeni katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Khalifa Haftar anajaribu kueneza wigo wa kimataifa wa mgogoro wa Libya
Jan 01, 2020 04:22Baada ya kupinduliwa utawala wa Muammar Gaddafi huko Libya mwaka 2011, nchi hiyo ilitumbukia katika vita vya ndani na hivi sasa kuna serikali mbili hasimu, moja ya mashariki na nyingine ya magharibi mwa nchi hiyo ambapo vikosi vya pande hizo mbili vinaendelea kupigana,
-
Umoja wa Mataifa walaani mashambulizi ya Haftar dhidi ya raia huko Libya
Dec 29, 2019 23:44Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametoa taarifa jana usiku akilaani mashambulizi ya anga yanayofanywa na kundi kwa jina la jeshi la kitaifa la Libya dhidi ya raia wa nchi hiyo chini ya uongozi wa Khalifa Haftar.
-
Uturuki yaonya kuhusu hatari ya Libya kugeuka kuwa Syria
Dec 29, 2019 09:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Mevlut Cavusoglu, ambaye nchi yake inajitayarisha kutuma wanajeshi Libya ameonya kuwa, kuendelea mgogoro wa Libya kwa muda mrefu kunaweza kuitumbukiza nchi hiyo katika hali mbaya zaidi na kuigeuza kuwa sawa na Syria.
-
Mawaziri wanne wa Ulaya kutembelea Libya
Dec 28, 2019 23:23Serikali ya Muafaka wa Kitaifa Libya imetangaza kuwa, mawaziri wa mambo ya nje wa Italia, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani wanatazamiwa kutembelea mji mkuu wa nchi hiyo, Tripoli.
-
Putin asisitiza ulazima wa kutatuliwa kwa amani mgogoro wa Libya
Dec 27, 2019 03:55Rais wa Russia amemhutubu na kumsisitizia Waziri Mkuu wa Italia kuwa mgogoro wa Libya unapasa kupatiwa ufumbuzi kwa njia ya amani.
-
Al Sisi: Misri inaunga mkono ufumbuzi wa kisiasa wa mgogoro wa Libya
Dec 26, 2019 22:53Rais wa Misri amesema kuwa nchi yake inataka kulinda ardhi kamili ya Libya na inakaribisha utatuzi wa kisiasa wa mgogoro wa nchi hiyo.
-
Rais Erdogan wa Uturuki afanya safari ya ghafla Tunisia kujadili usitishaji vita nchini Libya
Dec 26, 2019 04:22Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki jana alifanya safari ya ghafla nchini Tunisia kujadili namna ya kushirikiana na nchi hiyo ili kutafuta uwezekano wa kufanikisha usitishaji vita katika nchi jirani ya Libya, ambapo Ankara ni muungaji mkono wa serikali ya nchi hiyo inayotambuliwa rasmi kimataifa.