• Maelfu washiriki kwenye maandamano ya Morocco ya kuunga mkono Palestina

    Maelfu washiriki kwenye maandamano ya Morocco ya kuunga mkono Palestina

    Dec 25, 2023 06:30

    Maelfu ya watu nchini Morocco wamefanya mojawapo ya maandamano makubwa zaidi ya kuunga mkono Palestina mjini Rabat, tangu kuzuka kwa vita vya Gaza, wakati wakiitisha kuvunjwa kwa mahusiano kati ya taifa lao na Israel.

  • Watunisia wafanya maandamano makubwa mbele ya ubalozi wa Marekani kuiunga mkono Gaza

    Watunisia wafanya maandamano makubwa mbele ya ubalozi wa Marekani kuiunga mkono Gaza

    Dec 25, 2023 02:41

    Wananchi wa Tunisia jana Jumapili walifanya maandamano mkabala wa ubalozi wa Marekani katika mij mkuu wa nchi hiyo Tunis, kwa ajili ya kuiunga mkono Gaza. Wananchi wa Tunisia wamekuwa wakiandamana kwa ajili ya kuwaunga mkono raia wa Palestina wa Ukanda wa Gaza na kupinga mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni.

  • Watumishi wa umma Uholanzi waandamana wakitaka kusitishwa vita Gaza

    Watumishi wa umma Uholanzi waandamana wakitaka kusitishwa vita Gaza

    Dec 23, 2023 02:27

    Makumi ya wafanyakazi wa umma nchini Uholanzi jana Ijumaa waliwashangaza wengi kwa kuingia mabarabarani kushiriki maandamano ya kutaka kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu katika Ukanda wa Gaza.

  • Wayemen wafanya maandamano kulaani jinai za Wazayuni Gaza

    Wayemen wafanya maandamano kulaani jinai za Wazayuni Gaza

    Dec 15, 2023 10:17

    Wananchi wa Yemen kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano makubwa ya kulaani jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na vile vile kuonyesha mshikamano wao na taifa la Palestina.

  • Wacanada waandamana wakimtaka Trudeau aache kuiuzia Israel silaha

    Wacanada waandamana wakimtaka Trudeau aache kuiuzia Israel silaha

    Dec 13, 2023 11:15

    Waungaji mkono wa Palestina wanaoishi nchini Canada wamefanya maandamano makubwa kulaani jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, ambapo mbali na kuonyesha mshikamano wao na wakazi wa Gaza, lakini pia wamemtaka Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Justin Trudeau kuacha kuuuzia silaha utawala wa Kizayuni.

  • Wanigeria waandamana wakitaka kukatwa uhusiano na Israel

    Wanigeria waandamana wakitaka kukatwa uhusiano na Israel

    Dec 03, 2023 10:42

    Kwa mara nyingine tena, maelfu ya Waislamu na waungaji mkono wa Palestina katika mji wa Kano, kaskazini mwa Nigeria wameandamana na kulaani jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina hasa wa Ukanda wa Gaza.

  • Makumi ya maelfu ya Wamorocco waandamana wakitaka kukatwa uhusiano wa nchi hiyo na Tel Aviv

    Makumi ya maelfu ya Wamorocco waandamana wakitaka kukatwa uhusiano wa nchi hiyo na Tel Aviv

    Nov 28, 2023 05:15

    Makumi ya maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano makubwa ya kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kutaka kusitishwa juhudi za kuhuishwa uhusiano kati ya Rabat na Tel Aviv. Wafanya maandamano hao kwa mara nyingine tena wamelaani jinai za utawala haramu wa Israel na kutaka kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu huko Ukanda wa Gaza.

  • Wananchi wa Morocco waandamana kuwaunga mkono Wapalestina wa Gaza

    Wananchi wa Morocco waandamana kuwaunga mkono Wapalestina wa Gaza

    Nov 08, 2023 07:10

    Wananchi wa Morocco kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano ya kuwanga mkono wananchi wa Palestina ambao wanakabiliwa na hujuma na mashambulizi ya kikatili ya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.

  • Kuongezeka  upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi

    Kuongezeka upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi

    Nov 07, 2023 02:31

    Mwezi mmoja ukiwa umepita tangu kujiri operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na utawala wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi makali ya mabomu ambayo hajawahi kushuhudiwa tena huko Ghaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya Wapalestina, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake, mwenendo wa upinzani dhidi ya vitendo hivyo vya jinai vya Israeli, umeongezeka sana duniani ikiwa ni pamoja na nchini Marekani, ambayo ni mwitifaki mkubwa wa Tel Aviv.

  • Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yafanyika Ujerumani, Italia

    Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yafanyika Ujerumani, Italia

    Nov 05, 2023 13:41

    Maelfu ya watu wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin kushiriki maandamano ya kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina, huku idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi hadi sasa katika mashambulizi dhidi ya Ukanda wa Gaza ikipindukia 10,000.