-
Mamilioni ya watu washiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds kote duniani
Jul 01, 2016 03:23Mamilioni ya watu hapa Iran na katika nchi zingine kote duniani wanashiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds, kuonyesha uungaji mkono wao kwa wananchi madhulumu wa Palestina sambamba na kulaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika ardhi zao unazozikalia kwa mabavu.
-
Wairaqi waandamana kumuunga mkono Sheikh Qassim wa Bahrain
Jun 25, 2016 02:08Wananchi wa Iraq wamefanya maandamano ya kuonyesha uungaji mkono wao kwa mwanachuoni mkubwa wa Kiislamu Ayatullah Sheikh Isa Qassim ambaye hivi karibuni alivuliwa uraia na utawala wa Aal-Khalifa wa Bahrain.
-
HRW: Watu 400 wameuawa katika maandamano dhidi ya serikali Ethiopia
Jun 16, 2016 11:01Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema mamia ya watu wameuawa katika maandamano ya wananchi dhidi ya serikali ya Ethiopia, kuanzia Novemba mwaka jana hadi sasa.
-
Watu saba wauawa na kujeruhiwa Kenya
Jun 06, 2016 23:11Mapigano kati ya vikosi vya usalama na waandamanaji katika mji wa Kisumu Kenya yamesababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine sita.
-
Walowezi wa Kizayuni wafanya maandamano Quds, wavamia al-Aqsa
Jun 06, 2016 02:59Maelfu ya walowezi wa Kizayuni wamefanya maandamano ya kutiliwa shaka mashariki mwa Quds inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel na kuzusha hali ya taharuki katika eneo hilo.
-
Wafuasi wa upinzani DRC kuandaa maandamano Kinshasa leo
May 25, 2016 22:55Vyombo vya usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimeupa idhini muungano wa vyama vya upinzani nchini humo kuandaa maandamano katika mji mkuu Kinshasa hii leo.
-
Maelfu waandamana Zimbabwe kumuunga mkono Mugabe
May 25, 2016 10:02Maelfu ya wananchi wa Zimbabwe wamejitokeza barabarani katika mji mkuu Harare, kushiriki maandamano ya kuonyesha uungaji mkono wao kwa rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe, mwenye umri wa miaka 92.
-
Watu watatu wafariki dunia nchini Kenya katika maandamano ya wapinzani wa serikali
May 23, 2016 23:12Watu watatu wamepoteza maisha yao na wengine kadhaa kujeruhiwa nchini Kenya baada ya maandamano ya mrengo wa upinzani ya kutaka Tume ya Uchaguzi na Mipaka IEBC ijiuzulu kugeuka na kuwa uwanja wa fujo.
-
Wafungwa wa Misri wasusia chakula kukosoa 'kesi bandia'
May 23, 2016 07:47Makumi ya wafungwa wa Misri walioshiriki maandamano ya kuikosoa serikali ya Cairo kwa kuipa Saudi Arabia visiwa viwili vinavyomilikiwa na nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika wanafanya mgomo wa kula, kulalamikia kile walichokitaja kuwa kesi bandia na za kidhulma dhidi yao.
-
Upinzani Kenya: Wabunge wa Jubilee wanapanga njama ya kuahirisha uchaguzi mkuu 2017
May 22, 2016 23:03Viongozi wa upinzani nchini Kenya wamedai wabunge wa muungano tawala wa Jubilee wanapanga njama ya kuvuruga maandamano yao ya amani ambayo hufanyika kila Jumatatu kwa lengo la kushinikiza kujiuzulu makamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC, ili itangaze hali ya hatari na hatimaye kuahirisha uchaguzi mkuu unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao wa 2017.