Askari wanne na raia watatu wa Uganda wameripotiwa kuuawa katika mapigano makali baina ya vikosi vya majini vya Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika maji ya Ziwa Albert.
Watu wasiopungua kumi wameuawa katika mapigano ya kikabila yaliyotokea magharibi mwa Ethiopia.
Baraza la Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Ulaya limesisitiza kuwa, mgogoro wa Yemen hauwezi kupatiwa ufumbuzi kwa njia za kijeshi na kwamba, ufumbuzi pekee ni kupatikana amani ya kudumu kupitia njia ya mazungumzo.
Gavana wa jimbo la Plateau lililoko katikati mwa Nigeria amesema idadi ya watu waliouawa katika mapigano ya kikabila yaliyofanyika mwishoni mwa wiki imepindukia watu 200.
Watu kadhaa wameuawa na kujeruhiwa katika mapigano mapya yaliyotokea katika mji wa Sabha, kusini magharibi mwa Libya.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani ametoa wito wa kukomeshwa mapigano, machafuko pamoja na vitendo vya utumiaji mabavu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Wimbi jipya la mapigano katika Rasi ya Sinai nchini Misri limepelekea kuuawa wapiganaji 16 wa kundi la kigaidi na wanajeshi wawili wa serikali.
Kwa akali watu 22 wameuawa kwenye mapigano ya kikabila mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Watu zaidi ya 30 wameuawa katika mapigano ya kikabila yaliyotokea katika mkoa wa Ituri huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mapigano mapya kati ya jeshi na waasi yameripotiwa karibu na mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba, siku chache baada ya kuvurugika kwa makubaliano ya amani yaliyosainiwa kati ya pande hasimu za kisiasa mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.