-
Iran yalaani shambulizi dhidi ya Waislamu msikitini Afrika Kusini
May 12, 2018 03:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali shambulizi la hivi karibuni dhidi ya msikiti mmoja karibu na mji wa Durban nchini Afrika Kusini.
-
Mashambulizi pacha ya mabomu yaua kadhaa msikitini Nigeria
Apr 22, 2018 09:31Mashambulizi pacha ya mabomu yameua waumini watatu wa Kiislamu msikitini katika mji wa Bama jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Mzozo wa uongozi wapelekea msikiti kufungwa na kuzingirwa Uganda
Mar 23, 2018 02:52Wanajeshi na maafisa wa polisi wameufunga na kuuzingira Msikiti wa Basajjabalaba katika Manispaa ya Bushenyi-Ishaka magharibi mwa Uganda kutokana na mzozo miongoni mwa Waislamu katika eneo hilo.
-
Msikiti mwingine washambuliwa kwa bomu nchini Ujerumani
Mar 20, 2018 12:23Msikiti mmoja katika mji wa Ulm, kusini mwa Ujerumani umeshambuliwa kwa bomu na watu wasiojulikana, chini ya wiki mbili baada ya msikiti mwingine kuteketezwa kwa moto katika mji mkuu wa nchi hiyo ya Ulaya, Berlin.
-
Maadui watangaza "Siku ya Kumwadhibu Muislamu" nchini Uingereza
Mar 11, 2018 23:00Taharuki imetanda miongoni mwa Waislamu nchini Uingereza baada ya kundi lenye chuki dhidi ya Uislamu kusambaza barua za kutaka kushambuliwa Waislamu na misikiti nchini humo.
-
Wenye chuki dhidi ya Uislamu wachoma moto msikiti nchini Ujerumani
Mar 11, 2018 12:58Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa matukio ya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu barani Ulaya, wavamizi wasiojulikana wameuteketeza moto msikiti mmoja katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin.
-
Saudia yahujumu na kuvunja misikiti katika mashambulio yake mapya nchini Yemen
Feb 25, 2018 12:06Ndege za kivita za utawala wa Aal-Saud zimelenga misikiti na vituo vingine vya Kiislamu katika hujuma zake mpya za anga nchini Yemen.
-
Waziri Mkuu wa Uingereza atembelea msikiti akiwa amevaa mtandio kichwani
Feb 19, 2018 12:09Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametembelea msikiti mmoja mjini London akiwa amevaa mtandio kichwani ikiwa ni sehemu ya kushiriki katika kampeni maalumu ya Waislamu wa Uingereza inayoendeshwa chini ya kaulimbiu ya "Tembelea Msikiti Wangu."
-
Waislamu wazidi kunyanyaswa barani Ulaya; msikiti wachomwa moto Uholanzi
Feb 12, 2018 04:19Ikiwa ni katika kuendeleza vitendo vya unyanyasaji dhidi ya Waislamu, watu wenye chuki za kidini wameuchoma moto msikiti mmoja katika mji wa Drachten wa kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Hujuma ya kigaidi msikitini Benghazi, Libya, watu kadhaa wauawa au kujeruhiwa
Feb 09, 2018 11:48Watu kadhaa wanaripotiwa kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mji wa Benghazi nchini Libya kufuatia hujuma ya kigadi wakati wa Sala ya Ijumaa hii leo.