Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali shambulizi la hivi karibuni dhidi ya msikiti mmoja karibu na mji wa Durban nchini Afrika Kusini.
Mashambulizi pacha ya mabomu yameua waumini watatu wa Kiislamu msikitini katika mji wa Bama jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Wanajeshi na maafisa wa polisi wameufunga na kuuzingira Msikiti wa Basajjabalaba katika Manispaa ya Bushenyi-Ishaka magharibi mwa Uganda kutokana na mzozo miongoni mwa Waislamu katika eneo hilo.
Msikiti mmoja katika mji wa Ulm, kusini mwa Ujerumani umeshambuliwa kwa bomu na watu wasiojulikana, chini ya wiki mbili baada ya msikiti mwingine kuteketezwa kwa moto katika mji mkuu wa nchi hiyo ya Ulaya, Berlin.
Taharuki imetanda miongoni mwa Waislamu nchini Uingereza baada ya kundi lenye chuki dhidi ya Uislamu kusambaza barua za kutaka kushambuliwa Waislamu na misikiti nchini humo.
Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa matukio ya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu barani Ulaya, wavamizi wasiojulikana wameuteketeza moto msikiti mmoja katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin.
Ndege za kivita za utawala wa Aal-Saud zimelenga misikiti na vituo vingine vya Kiislamu katika hujuma zake mpya za anga nchini Yemen.
Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametembelea msikiti mmoja mjini London akiwa amevaa mtandio kichwani ikiwa ni sehemu ya kushiriki katika kampeni maalumu ya Waislamu wa Uingereza inayoendeshwa chini ya kaulimbiu ya "Tembelea Msikiti Wangu."
Ikiwa ni katika kuendeleza vitendo vya unyanyasaji dhidi ya Waislamu, watu wenye chuki za kidini wameuchoma moto msikiti mmoja katika mji wa Drachten wa kaskazini mwa nchi hiyo.
Watu kadhaa wanaripotiwa kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mji wa Benghazi nchini Libya kufuatia hujuma ya kigadi wakati wa Sala ya Ijumaa hii leo.