Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri imesema kuwa, kuna uwezekano makundi ya kigaidi yakafanya tena mashambulizi nchini humo, hivyo imevitaka vikosi vya usalama kuchukua hatua kali za kiusalama kukabiliana na jambo hilo.
Watu wasiopungua 28 waliuawa nchini Misri na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia shambulio la jana Ijumaa dhidi ya mabasi mawili yaliyokuwa yamewabeba Wakristo wa Kibti kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo Cairo.
Kwa akali maafisa watano wa polisi nchini Kenya wameuawa katika shambulizi la bomu lililotokea leo Alkhamisi eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
Kwa akali watu 36 wameuawa katika shambulizi la kigaidi dhidi ya kambi ya wakimbizi lililofanywa jana Jumanne na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, kaskazini mashariki mwa Syria.
Wanajeshi wanane wameuawa katika mlipuko wa bomu uliotokea katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia.
Polisi ya Ufaransa imetangaza kuwa, mtu aliyehusika na shambulizi la jana mjini Paris alikuwa na historia ya uhalifu na kufungwa jela.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya mabomu dhidi ya mabasi yaliyokuwa yanawahamisha watu kutoka vijiji ambavyo aghalabu ya wakazi wake ni Waislamu wa madhehebu ya Shia huko katika mkoa wa Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria.
Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amelaani vikali mashambulizi ya kigaidi dhidi ya makanisa mawili nchini Misri siku ya Jumapili iliyopita ambapo makumi ya watu waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa huku akisisitiza kuwa, lengo la magaidi ni kuzusha mifarakano ya kidini duniani.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya kigaidi dhidi ya makanisa mawili nchini Misri hapo jana, ambapo makumi ya watu waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Watu wasiopungua 15 wameuawa baada ya bomu lililotegwa ndani ya gari kuripuka nje ya kambi ya jeshi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.