-
HRW: US kushadidisha hujuma zake za anga Somalia kunahatarisha usalama wa raia
Apr 02, 2017 03:42Hatua ya Marekani ya kuidhinisha kushadidishwa mashambulizi yake ya anga dhidi ya ngome za kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab nchini Somalia imekosolewa vikali na asasi za kutetea za haki za binadamu.
-
UN: Malaki ya raia wa Somalia wamekuwa wakimbizi miezi 4 ya hivi karibuni
Mar 31, 2017 22:29Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, malaki ya watu nchini Somalia wamelazimika kuwa wakimbizi katika miezi minne ya hivi karibuni kutokana na ukame na baa la njaa.
-
HRW yakosoa shambulio la Saudia dhidi ya wakimbizi wa Kisomali
Mar 27, 2017 08:10Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW) limelitaja shambulio lililofanywa hivi karibuni na utawala wa Saudi Arabia dhidi ya boti iliyokuwa imewabeba wakimbizi wa Kisomali karibu na pwani ya Yemen kuwa ni jinai ya kivita.
-
IGAD yaafiki kusaidia kuwarejesha nyumbani wakimbizi wa Somalia
Mar 26, 2017 09:12Shirika la Kiserikali la Ustawi wa nchi za Mashariki mwa Afrika IGAD limeafiki kusaidia kuwarejesha kwa hiari katika nchi yao wakimbizi wa Somalia.
-
Maharamia wa Somalia wateka nyara meli ili kuitumia kuendeshea mashambulizi
Mar 24, 2017 10:50Maharamia wameteka nyara meli moja ya uvuvi ya Somalia ili kuitumia kama kituo cha kuendeshea mashambulizi dhidi ya meli kubwa. Hayo yameelezwa leo na polisi ya Somalia wiki moja baada ya maharamia wa nchi hiyo kuteka nyara meli ya kwanza ya kibiashara tangu mwaka 2012.
-
UN yaitaka jamii ya kimataifa kukabiliana na tatizo la njaa nchini Somalia
Mar 23, 2017 12:18Kwa mara nyingine Umoja wa Mataifa umeitaka jamii ya kimataifa kukabiliana na tatizo la njaa lililoikumba Somalia.
-
Msalaba Mwekundu: Dunia ina miezi 3 kunusuru mamilioni wanaokabiliwa na njaa Somalia, Yemen
Mar 22, 2017 11:41Shirika la Msalaba Mwekundu limeonya kuwa, jamii ya kimataifa ina miezi mitatu hadi minne kuokosoa maisha ya mamilioni ya watu wanaokabiliwa na baa la njaa katika nchi za Somalia na Yemen.
-
Waziri Mkuu Mpya wa Somalia atangaza baraza jipya la mawaziri 26
Mar 21, 2017 10:48Waziri Mkuu Mpya wa Somalia leo ametangaza baraza lake la mawaziri 26 na kumteua waziri wa zamani wa mambo ya nje kuwa Waziri wa Fedha huku akimteuwa pia mwandishi wa habari wa BBC kuwa mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa nchi hiyo.
-
Waziri Mkuu wa Somalia: Saudia, mhusika wa mauaji ya wakimbizi wa Kisomali
Mar 20, 2017 11:38Serikali ya Somalia imesema kuwa utawala wa Saudi Arabia ndio uliohusika na mauaji ya wakimbizi wa nchi hiyo katika maji ya Yemen.
-
Saudia yaitaka UN isimamie bandari ya Yemen baada ya kuua kikatili Wasomali 44
Mar 20, 2017 04:31Muungano vamizi wa kijeshi wa Saudi Arabia nchini Yemen umeutaka Umoja wa Mataifa uchukue udhibiti wa bandari ya Hudaydah baada ya helikopta ya Aal-Saud aina ya Apache kufanya shambulio la kikatili dhidi ya boti ya wakimbizi karibu na Lango Bahari la Bab al-Mandab, pwani ya Yemen na kuua makumi ya raia wa Somalia.