-
Maadui wa ash Shabab wateka mji Somalia
Oct 26, 2016 13:01Maafisa wa serikali wa Somalia wamethibitisha habari iliyosema kuwa, kundi moja la wapinzani wa ash Shabab ambalo linaliunga mkono kundi la kigaidi la Daesh, limeteka mji mmoja wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
UN: Maelfu ya Wasomalia wakimbia mapigano, mvua zinatishia maisha yao
Oct 25, 2016 02:27Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, zaidi ya watu elfu 75 wamekimbia makazi yao na wengine 18 wameuawa katika wiki tatu za mapigano yanayoendelea nchini Somalia.
-
Mripuko wa Bomu wautikisa mji wa Mogadishu
Oct 24, 2016 04:19Mtu moja ameuawa na wengine wawili wamejeruhiwa katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu wakati bomu lilipolipuka jana Jumapili, karibu na kambi ya wakimbizi.
-
AU yafanya uchunguzi kuhusu vitendo vya wanajeshi wake Somalia
Oct 22, 2016 03:44Umoja wa Afrika AU umesema, umeanzisha uchunguzi wa kubaini ni katika mazingira gani, askari wa kikosi cha AMISOM nchini Somalia walifanya mauaji dhidi ya raia.
-
Ash-Shabab wafanya shambulio karibu na mji mkuu wa Somalia na kuua watu 10
Oct 19, 2016 04:33Kundi la kigaidi na kitakfiri la ash-Shabab nchini Somalia limefanya shambulizi katika mji wa kistratijia ulio karibu na mji mkuu wa nchi hiyo, Mogadishu.
-
Umoja wa Afrika (AU) watilia mkazo kurejeshwa amani ya kudumu Somalia
Oct 16, 2016 04:21Kikosi cha kudumisha amani cha Umoja wa Afrika huko Somalia (AMISOM) kimesisitiza kuhusu sualal la kurejesha amani ya kudumu katika maeneo yote ya nchi hiyo.
-
UN: Wakimbizi 70,000 wa Dadaab wanataka kurudu Somalia
Oct 04, 2016 04:32Umoja wa Mataifa umesema robo ya wakimbizi wa Kisomali wanaoishi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya wametangaza utayarifu wao wa kurejea nchini kwao Somalia karibuni hivi.
-
UNHCR imewarejesha wakimbizi zaidi ya 30,000 wa Somalia kutoka Kenya
Sep 30, 2016 04:26Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limesema kuanzia mwezi Desemba mwaka 2014 wakimbizi zaidi ya elfu 30 wa Somalia wamerejeshwa kwa hiari katika nchi yao kutoka kambi ya wakimbizi ya Dadaab iliyoko kaskazini mashariki mwa Kenya.
-
Marekani yadai kufanya makosa katika kuwaua askari 22 wa Somalia
Sep 29, 2016 03:42Askari wa Marekani wametuhumiwa kuhusika na mauaji ya askari 22 wa Somalia katika kile kinachodaiwa kuwa ni makosa yaliyofanyika katika urushaji makombora ya ndege kaskazini mwa nchi hiyo ya Kiafrika.
-
Mjumbe wa UN alaani mauaji ya mwandishi habari Somalia
Sep 29, 2016 01:08Mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Michael Keating amelaani vikali mauaji ya mwandishi wa habari wa Radio Shabelle Abdiaziz Mohamed Ali yaliyotekelezwa Jumanne na watu wasiojulikana mjini Mogadishu Somalia.