-
Kufufuka uhusiano wa Iran na Sudan kwaitia wahka mkubwa Marekani
Feb 25, 2024 02:54John Godfrey, balozi wa Marekani nchini Sudan, amesema katika taarifa ya uingiliaji wa wazi wa mambo yasiyomuhusu ndewe wala sikio kwamba eti ana wasiwasi wa kuimarika uhusiano kati ya Iran na Sudan kwa madai kuwa uhusiano huo utaifanya Iran iisaidie kijeshi Sudan.
-
UN: Makumi ya watu wamebakwa, kunyanyaswa kingono nchini Sudan
Feb 23, 2024 22:44Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema katika ripoti yake mpya iliyotolewa jana Ijumaa kwamba makumi ya watu, wakiwemo watoto, wamekuwa waathiriwa wa ubakaji na aina nyingine za unyanyasaji wa kingono katika mzozo unaoendelea nchini Sudan, vitendo ambavyo vinaweza kutambuliwa kuwa ni uhalifu wa kivita.
-
Le Monde: Hakuna matumaini ya kukomeshwa vita hivi karibuni nchini Sudan
Feb 11, 2024 08:37Ripoti iliyochapishwa na gazeti la Ufaransa la Le Monde imesema kwamba, baada ya zaidi ya miezi 9 ya vita kati ya Jeshi la Sudan linaloongozwa na Abdel Fattah al-Burhan na Vikosi vya Msaada wa Haraka chini ya uongozi wa Mohamed Hamdan Dagalo, hakuna uwezekano wa kumalizika vita hivyo karibuni.
-
Mkurugenzi wa kampuni ya mawasiliano ya simu: RSF imekata mawasiliano kote Sudan
Feb 10, 2024 03:52Afisa wa huduma za mawasiliano wa Sudan amesema Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) ndivyo vinavyohusika na kukatika mawasiliano kote Sudan kwa siku ya nne mfululizo.
-
Sudan yakanusha taarifa za UN kuhusu Al-Burhan kukubali kukutana na Hemedti nchini Uswisi
Feb 09, 2024 04:40Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Sudan jana Alhamisi ilikanusha taarifa iliyotolewa na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffiths, ambaye alidokeza kuwa Rais wa Baraza Kuu la Utawala nchini Sudan, Jenerali Abdel Fattah Al-Burhan, amekubali kukutana na Kamanda wa Kikosi cha Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), nchini Uswisi, kwa madhumuni ya kuwezesha kuwasili kwa misaada kwa watu walioathirika na vita huko Sudan.
-
MSF: Watoto 13 wanaaga dunia kila siku kambini Darfur, Sudan
Feb 06, 2024 07:29Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imesema kwa akali watoto 13 wanafariki dunia kila siku kutokana na utapiamlo wa kiwango cha juu katika kambi moja ya wakimbizi nchini Sudan.
-
Rais Raisi: Sera ya msingi ya Iran ni kuunga mkono nchi zinazojitenga na Israel
Feb 05, 2024 23:30Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema sera ya msingi ya Jamhuri ya Kiislamu ni kuunga mkono nchi zinazojitenga na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Amir Abdollahian: Ni muhimu kufunguliwa tena balozi za Iran na Sudan ili kupanua ushirikiano
Feb 05, 2024 12:04Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa suala la kufunguliwa tena balozi za Iran na Sudan na kurejea shughuli za mabalozi wa nchi hizo mbili kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano wa pande zote lina umuhimu mkubwa, na kueleza kwamba kuna matumaini ya kustawishwa zaidi ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
-
ICC: Tunaamini pande zote mbili za vita nchini Sudan zimefanya uhalifu wa kivita Darfur
Jan 30, 2024 08:00Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, Karim Khan, ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba kuna "sababu za kuamini" kwamba jeshi la Sudan, Vikosi vya Msaada wa Haraka, na vikundi washirika wao wamefanya uhalifu wa kivita huko Darfur.
-
EU yayawekea vikwazo makampuni sita yanayodaiwa kuhusika katika kufadhili vita Sudan
Jan 22, 2024 23:51Baraza la Ulaya limeidhinisha vikwazo kwa makampuni sita yanayodaiwa kuhusika katika kufadhili vita nchini Sudan, ambapo vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo (SAF) na Wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) wamekuwa wakipigana tangu Aprili mwaka jana.