-
Vita vyawalazimisha watoto milioni mbili Sudan Kusini kukimbia makazi yao
May 08, 2017 10:55Umoja wa Mataifa umetangaza leo kuwa vita na ukame vimewalazimisha watoto zaidi ya milioni mbili kuyahama makazi yao nchini Sudan Kusini huku watu 21 wakiuawa katika shambulio la karibuni lililofanywa na watu wenye silaha wasiojulikana.
-
UN: Watoto milioni 2 wa Sudan Kusiniwamelazimika kuwa wakimbizi
May 08, 2017 03:18Umoja wa Mataifa umesema watoto zaidi ya milioni 2 wa Sudan Kusini wamelazimika kuyahama makazi yao kutokana na mapigano na ukame vinavyoisakama nchi hiyo changa zaidi barani Afrika.
-
UN yalaani shambulizi dhidi ya askari wa kusimamia amani huko Sudan Kusini
May 07, 2017 23:01Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, limelaani shambulizi la hivi karibuni la waasi wa Sudan Kusini dhidi ya askari wa kusimamia amani wa umoja huo katika mji wa Leer, magharibi mwa mkoa wa Upper Nile.
-
Umoja wa Mataifa waonyesha wasiwasi wake kutokana na kuendelea machafuko Sudan Kusini
May 05, 2017 09:09Mkuu wa Kamisheni ya Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameonyesha wasiwasi mkubwa alionao kutokana na kuendelea mgogoro wa Sudan Kusini na ametoa wito wa kusimamishwa mapigano katika nchi hiyo changa zaidi barani Afrika.
-
Uingereza yatuma mamia ya askari wake nchini Sudan Kusini
May 03, 2017 03:14Serikali ya Uingereza imeanza kutuma askari 400 wa nchi hiyo nchini Sudan Kusini kwenda kujiunga na Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa UNMISS.
-
Sudan Kusini yaipiga marufuku televisheni ya 'Aljazeera' nchini humo
May 02, 2017 03:48Ofisi ya kusimamia vyombo vya habari nchini Sudan Kusini, imezifunga ofisi za televisheni ya Al-Jazeera ya Kingereza kuendelea na shughuli zake ndani ya nchi hiyo.
-
AU yaonyesha masikitiko yake makubwa juu ya kuendelea mapigano Sudan Kusini
May 01, 2017 09:36Umoja wa Afrika umeonyesha wasi wasi wake mkubwa kutokana na hali mabaya nchini Sudan Kusini na kuendelea mapigano sambamba na mashambulizi dhidi ya raia wa kawaida.
-
UN yasema machafuko mapya Sudan Kusini yanaongeza mateso kwa raia
Apr 30, 2017 03:01Umoja wa Mataifa umeeleza kusikitishwa na kuongezeka kwa machafuko na mateso kwa raia wa Sudan Kusini, kufuatia operesheni ya hivi karibuni ya jeshi la serikali ya nchi hiyo.
-
Baadhi ya marais wa Afrika hawataki Machar arejee Sudan Kusini
Apr 27, 2017 03:32Mjumbe wa Umoja wa Mataifa amesema baadhi ya nchi za kanda ya Afrika Mashariki pamoja na Afrika Kusini haziungi mkono wazo la kurejea mjini Juba, kiongozi wa waasi nchini Sudan Kusini, Riek Machar.
-
Sudan yamtuhumu Rais wa Sudan Kusini kwa kufanya mazungumzo na waasi
Apr 25, 2017 03:46Sudan jana iliitaka nchi jirani ya Sudan Kusini isitishe uungaji mkono wake kwa makundi ya waasi wanaopigana vita na Khartoum na kumtuhumu Rais Kiir kuwa amekutana na kufanya mazungumzo na waasi wiki iliyopita.