Shirika la Afya Duniani WHO limesema watu takriban milioni 50 kote ulimwenguni wanaugua ugonjwa wa kusahau (Dementia) huku idadi hii ikitabiriwa kuongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2050.
Viongozi wa idara ya Msumbiji wametangaza kwamba zaidi ya watu 1000 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu nchini humo.
Wizara ya Afya ya Yemen imetangaza kuwa tangu mwaka mmoja uliopita hadi sasa watu 141 wameaga dunia kwa ugonjwa wa dondakoo; wengi wakiwa ni watoto wadogo.
Seneta wa jimbo la Vermont nchini Marekani, Bernie Sanders amemkosoa vikali Rais Donald Trump wa nchi hiyo kwamba, anawahadaa wapiga kura kwa kuwaambia uongo.
Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi Kusini mwa Afrika (SADC) zimekubaliana kushirikiana kupambana na ugonjwa wa listeriosis ulioibuka nchini Afrika Kusini.
Gazeti la Daily Mail linalochapishwa nchini Uingereza limeripoti kuwa watu 231 wamefariki dunia nchini humo kutokana na maambukizi ya kirusi cha homa ya mafua.
Takwimu zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani WHO kuhusu usugu wa viuavijasumu au antibiotics zinaonyesha kuwa juu sana kiwango cha usugu wa dawa hizo dhidi ya maradhi kadhaa yanayosababishwa na bakteria kote duniani.
Mwanabiolojia Muirani, kwa mara ya kwanza duniani, amevumbua njia ya kuwezesha kutibu ugonjwa wa Mfumo wa Neva (Multiple Sclerosis) maarufu kama MS.
Kundi Moja la Kimataifa la Utoaji Misaada limetahadharisha kuwa hadi kufikia mwisho wa mwaka huu idadi ya watoto wataoaga dunia kwa magonjwa na njaa vilivyosababishwa na vita huko Yemen watafikia zaidi ya elfu 50.
Umoja wa Mataifa na jumuiya za misaada ya kibinadamu zimeonya kwamba kipindupindu kinaenea kwa kasi katika maeneo yaliyoathirika na ukame nchini Somalia wakati nchi hiyo ikiendelea kunyemelewa na hatari kubwa ya baa la njaa.