-
UN yaitisha mkutano wa kwanza kujadili masuala ya bahari
Jun 02, 2017 22:00Umoja wa Mataifa umeandaa mkutano wa kwanza wa mambo ya baharini kuanzia tarehe 5 hadi 9 mwezi huu wa Juni, ili kubadilisha mwelekeo wa hali inayozidi kuwa mbaya ya mazingira ya ikolojia baharini, na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu ya mambo ya bahari.
-
Wahajiri 58 wafa maji bahari ya Mediterrania, 100 watoweka
May 30, 2017 11:03Umoja wa Mataifa umesema wahajiri 58 aghalabu yao wakiwa ni watoto wadogo wamekufa maji katika Bahari ya Mediterrania karibu na pwani ya Libya wakijaribu kuingia barani Ulaya.
-
UN yaunda timu ya kuchunguza jinai dhidi ya Waislamu wa Rohingya
May 30, 2017 10:59Umoja wa Mataifa umeunda timu ya wataalamu huru kuchunguza mauaji na jinai zinazofanywa na jeshi la Myanmar dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya katika jimbo la Rakhine.
-
UN yaonya kuhusu kuendelea mapigano Jamhuri ya Afrika ya Kati
May 29, 2017 02:48Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusu kuanza upya mapigano ya kikabila na kidini katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
-
UN yatahadharisha kuhusu kusimamishwa misaada ya kibinadamu nchini Nigeria
May 25, 2017 23:24Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa, kupunguzwa bajeti za umoja huo kumezikwamisha taasisi zake katika kuendesha miradi mbalimbali ya kimataifa ikiwa ni pamoja na kuwatumia chakula waathirika wa mashambulizi ya kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Ukosoaji mkali wa UN kwa uamuzi wa Marekani wa kupunguza bajeti ya mchango wake kwa umoja huo
May 25, 2017 21:55Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stéphane Dujarric, amesema pendekezo la serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani la kupunguza bajeti ya mchango wa nchi hiyo kwa umoja huo litaufanya uendeshaji wa shughuli za taasisi hiyo ya kimataifa liwe jambo "lisiloyumkinika".
-
UN yaeleza wasi wasi wake kuhusu hali ya mateka wa Palestina
May 25, 2017 09:21Umoja wa Mataifa umeeleza wasi wasi wake kuhusu hali ya kiafya ya mateka wa Kipalestina waliosusia chakula katika magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Libya yataka kuondolewa vikwazo vya silaha
May 24, 2017 09:55Waziri Mkuu wa serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya ametaka nchi yake iondolewe vikwazo vya silaha.
-
Askari 2 wa kulinda amani wa UN wauawa nchini Mali
May 24, 2017 03:17Askari wawili wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa nchini Mali wameuawa katika uvamizi wa genge la kitakfiri lenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda kaskazini mwa nchi.
-
Myanmar yapinga ripoti ya UN kuhusu jinai zake dhidi ya Waislamu wa Rohingya
May 23, 2017 03:15Jeshi la Myanmar limekanusha ripoti ya uchunguzi wa Umoja wa Mataifa iliyosema kuwa viongozi wa serikali wanabeba dhima ya jinai zilizotendwa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya.