-
Umoja wa Mataifa: Maradhi ya kipindupindu yameenea kila kona ya Yemen
Jun 09, 2017 23:26Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, maradhi ya kipindipindu yameenea katika kila kona ya Yemen huku hali ya kibinadamu katika nchi hiyo ikiripotiwa kuzidi kuwa mbaya siku baada ya siku.
-
UN yataka kusitishwa mshambulizi dhidi ya raia huko CAR
Jun 09, 2017 03:37Kikosi cha wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati kimetoa wito wa kusimamishwa haraka iwezekanavyo mashambulizi yanayofanywa na makundi yenye silaha dhidi ya raia wa nchi hiyo.
-
AU, UN zataka kupunguzwa askari wa kulinda amani Darfur, Sudan
Jun 07, 2017 03:03Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa zimependekeza kupunguzwa idadi ya askari wanaohudumu kwenye Kikosi cha pamoja cha AU na UN huko Darfur, nchini Sudan UNAMID.
-
UN: Daesh imeua raia 163 waliokuwa wakikimbia Mosul, Iraq
Jun 06, 2017 23:18Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh limeua raia 163 waliokuwa wakiukimbia mji wa Mosul nchini Iraq ndani ya wiki moja pekee.
-
UN yaipa DRC siku 2 ichunguze mauaji na jinai eneo la Kasai
Jun 06, 2017 09:06Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameipa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku mbili ionyeshe azma na irada ya kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji na jinai za kibinadamu katika eneo la Kasai.
-
Marekani yatishia kujiondoa kwenye Baraza la Haki za Binadamu la UN
Jun 05, 2017 22:57Marekani inatazamiwa kutoa ishara leo Jumanne juu ya uwezekano wa kujiondoa kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuukingia kifua utawala haramu wa Israel.
-
Kubariki Umoja wa Mataifa njama zinazotekelezwa na Saudia nchini Yemen
Jun 04, 2017 21:47Harakati ya Ansarullah ya Yemen imekosoa pendekezo la mjumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu kukabidhi udhibiti wa bandari ya Al-Hudayda kwa upande mwengine wa tatu usioegemea upande wowote.
-
UN yaitisha mkutano wa kwanza kujadili masuala ya bahari
Jun 02, 2017 22:00Umoja wa Mataifa umeandaa mkutano wa kwanza wa mambo ya baharini kuanzia tarehe 5 hadi 9 mwezi huu wa Juni, ili kubadilisha mwelekeo wa hali inayozidi kuwa mbaya ya mazingira ya ikolojia baharini, na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu ya mambo ya bahari.
-
Wahajiri 58 wafa maji bahari ya Mediterrania, 100 watoweka
May 30, 2017 11:03Umoja wa Mataifa umesema wahajiri 58 aghalabu yao wakiwa ni watoto wadogo wamekufa maji katika Bahari ya Mediterrania karibu na pwani ya Libya wakijaribu kuingia barani Ulaya.
-
UN yaunda timu ya kuchunguza jinai dhidi ya Waislamu wa Rohingya
May 30, 2017 10:59Umoja wa Mataifa umeunda timu ya wataalamu huru kuchunguza mauaji na jinai zinazofanywa na jeshi la Myanmar dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya katika jimbo la Rakhine.