-
UN yataka kuanza mazungumzo ya kitaifa Kongo
Jul 16, 2016 00:05Mkuu wa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani katika Jamhuri yqa Kidemokrasia ya Kongo ametilia mkazo udharura wa kufanyika mazungumzo ya kitaifa kwa ajili ya kuzuia kushadidi mgogoro nchini humo.
-
Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Sudan Kusini
Jul 11, 2016 08:28Wanachama 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wametoa taarifa wakitaka kuhitimishwa mapigano katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.
-
Umoja wa Mataifa watiwa wasiwasi na mapigano yanayoendelea Sudan Kusini
Jul 09, 2016 11:31Mapigano yaliyoshtadi katika siku kadhaa zilizopita huko Sudan Kusini yamemfanya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kueleza wasiwasi wake kutokana na machafuko yanayoendelea huko Juba mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Kenya yakanusha ripoti ya UN ya kuua raia 29 Somalia
Jul 08, 2016 23:51Kenya imekanusha vikali ripoti ya Umoja wa Mataifa inayodai kuwa Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo KDF liliua raia wapatao 29 katika hujuma ya anga iliyolifanya baada ya wanamgambo wa al-Shabaab kuvamia kambi ya jeshi hilo katika eneo la El-Adde nchini Somalia Januari mwaka huu na kuua idadi kubwa ya askari wa Kenya waliokuwa chini ya kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM).
-
UN yalaani mauaji ya wakili wa haki za binadamu Kenya
Jul 06, 2016 00:02Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imelaani vikali mauaji ya wakili wa haki za binadamu nchini Kenya Bwana Willie Kimani, mteja wake Josphat Mwenda, na dereva wao wa taxi Joseph Muiruri, yaliyofanyika Juni 23.
-
Sudan: Kuongezwa muda vikosi vya UNAMID ni mkinzano
Jul 01, 2016 03:29Kwa mara nyingine tena serikali ya Sudan imekosoa vikali hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuongeza muda wa kuhudumu vikosi vya kimataifa vya kusimamia amani huko Daruf UNAMID kwa mwaka mmoja zaidi.
-
UN yaongeza askari 2,500 wa kulinda amani nchini Mali
Jun 30, 2016 02:53Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeafiki kuongezwa askari 2,500 wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Mali MINUSMA ambapo kikosi hicho sasa kitakuwa na jumla ya askari jeshi 13,289 na askari polisi 1,920.
-
Wasiwasi kuhusu ukatili wa Israel dhidi ya watoto Wapalestina
Jun 26, 2016 02:50Kufuatia kushadidi ukatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watoto Wapalestina, kumekuwepo wasiwasi na malalamiko makubwa miongoni mwa Wapalestina na jamii ya kimataifa.
-
UN: Israel inafanya ukatili dhidi ya watoto wa Palestina
Jun 25, 2016 08:22Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake kuhusu ukatili unaofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watoto wa Kipalestina.
-
UN: Zaidi ya madaktari na wauguzi 700 wameuawa Syria
Jun 21, 2016 23:35Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa madaktari na wauguzi zaidi ya 700 wameuawa nchini Syria tangu nchi hiyo iliposhambuliwa na mamluki wanaosaidiwa na nchi kadhaa za kigeni miaka mitano iliyopita.