-
Wahajiri wanane wakutwa ndani ya lori la friji wakisafirishwa kupelekwa Uingereza
Oct 28, 2019 04:33Wahajiri wanane kutoka Afghanistan wamekutwa ndani ya lori la friji lililokuwa likielekea Uingereza, wakati lori hilo lilipokaguliwa katika bandari ya Calais nchini Ufaransa. Hayo ni kwa mujibu wa ofisi ya mkuu wa mashtaka wa mji huo.
-
Wahajiri tisa wafariki dunia, 22 waokolewa baada ya boti yao kuzama katika pwani ya Italia
Oct 07, 2019 15:34Watu wasiopungua tisa wamefariki dunia baada ya boti iliyokuwa imebeba makumi ya wahajiri kuzama katika pwani ya kisiwa cha Lampedusa, kusini mwa Sicily nchini Italia.
-
Gadi ya pwani ya Libya yaokoa makumi ya wahajiri
Sep 29, 2019 23:06Gadi ya Pwani ya Libya imetangaza kuwaokoa wahajiri haramu wapatao 70 baada ya boti yao kuzama katika bahari ya Mediterania.
-
Wahariji 155 wa Kiafrika wamiminika kaskazini mwa Morocco
Aug 30, 2019 22:12Viongozi wa eneo la Ceuta linalodhibitiwa na Uhispania lililoka kaskasini mwa Morocco wametangaza kuwa kundi moja kubwa la wahajiri wa Kiafrika limeingia kwenye eneo hilo kinyume cha sheria.
-
HRW yakosoa ukandamizaji wa Saudia dhidi ya wahajiri wa Kiethiopia
Aug 16, 2019 23:12Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeeleza wasiwasi wake kuhusu haki ya wahajiri wa Kiethiopia nchini Saudi Arabia na kukosoa ukiukwaji wa haki zao unaofanywa na maafisa wa nchi hiyo.
-
WHO: Dawa mbili zilizoko kwenye majaribio zimeonyesha uwezekano mkubwa kutibu Ebola
Aug 14, 2019 03:40Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kkuwa, Dawa mbili mpya zinazojaribiwa kwa wagonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimeonyesha kuwa, zina uwezo mkubwa wa kutibu maradhi hayo.
-
Rais wa zamani wa Gambia atuhumiwa kufanya mauaji dhidi ya wahajiri
Jul 24, 2019 22:10Rais wa zamani wa Gambia ametuhumiwa kwamba mwaka 2005 alitoa amri ya kutekelezwa mauaji ya umati dhidi ya wahajiri 30 pamoja na mwandishi mmoja wa habari.
-
Viwiliwili vya wahajiri 79 waliozama baharini Tunisia vyapatikana
Jul 13, 2019 08:06Siku kumi zilizopita, mtumbwi mmoja uliokuwa umejaza wahajirii ulizama karibu na fukwe za Tunisia. Hadi hivi sasa miili 79 ya wahajirii hao imeshaopolewa kutoka baharini.
-
Maelfu waandamana Marekani kupinga udhalilishaji wa Trump kwa wahajiri
Jul 13, 2019 07:59Maelfu ya watu wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya Marekani, kupinga sera hasi za utawala wa Rais Donald Trump dhidi ya wahajiri wanaozuiliwa katika vituo vya mpaka wa nchi hiyo, na pia dhidi ya mpango wa kuwakamata na kuwatimua nchi humo wahajiri ambao hawajasajiliwa.
-
HRW, Amnesty zataka kufungwa vituo vya kuwazuilia wahajiri Libya
Jul 12, 2019 10:48Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Human Rights Watch, Amnesty International na Baraza la Ulaya la Wakimbizi na Wahajiri (ECRE) yametoa mwito wa kufungwa kambi za kuwazuilia wakimbizi na wahajiri nchini Libya.