Takwimu zilizozusha taharuki; Kuwait ina walimu wanne tu wa Fizikia
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i24219-takwimu_zilizozusha_taharuki_kuwait_ina_walimu_wanne_tu_wa_fizikia
Mkuu wa kamati ya bajeti katika bunge la Kuwait, Adnan Abdulsamad ametahadhrisha kuwa hivi sasa kuna walimu wanne tu nchini humo wanaofundisha somo la Fizikia na kusisitiza kuwa idadi hiyo haikubaliki kwa namna yoyote.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jan 25, 2017 03:55 UTC
  • Takwimu zilizozusha taharuki; Kuwait ina walimu wanne tu wa Fizikia

Mkuu wa kamati ya bajeti katika bunge la Kuwait, Adnan Abdulsamad ametahadhrisha kuwa hivi sasa kuna walimu wanne tu nchini humo wanaofundisha somo la Fizikia na kusisitiza kuwa idadi hiyo haikubaliki kwa namna yoyote.

Waziri wa Elimu ya Juu wa Kuwait Muhammad Al-Faris naye pia ameashiria uhaba mkubwa wa walimu ilionao nchi hiyo katika masomo muhimu kama Fizikia na Hesabati na kupendekeza kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo serikali iwaajiri Wakuwaiti wasio na vitambulisho vya uraia wanaojulikana kama 'Bedoons'; kwa kuzingatia kuwa wengi miongoni mwao wanafaulu kwa kiwango cha juu lakini kutokana na utambulisho wao, vyuo vikuu vya nchi hiyo haviko tayari kuwapatia fursa za kuendelea na masomo ya juu.

Waziri wa Elimu Muhammad al-Faris

Akizungumzia suala hilo, Abdulsamad amesema ni heri kuwapa mafunzo na kuwatumia Bedoons kuliko kuajiri walimu kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kutatua tatizo la uhaba wa walimu.

Nchini Kuwait kuna idadi ya Waarabu zaidi ya laki mbili waishio majangwani wanaojulikana kama Bedoons. Serikali ya Kuwait inawachukulia waarabu hao kuwa ni watu wasio na utambulisho na haiko tayari kuwapatia uraia wa nchi hiyo…/