Mtaalamu: Hizbullah itaibuka mshindi katika vita vyovyote na Israel
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i38617-mtaalamu_hizbullah_itaibuka_mshindi_katika_vita_vyovyote_na_israel
Uwezo wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon katika nyuga tofauti zikiwemo za kijeshi, vita stadi na vita vya kisaikolojia umeutia kiwewe utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kiasi cha kuwafanya weledi wa masuala ya kivita kusema kwamba, vita vyovyote vitakavyojiri kati ya Israel na harakati hiyo, vitamalizika kwa ushindi wa Hizbullah.
(last modified 2026-01-14T08:12:18+00:00 )
Jan 06, 2018 23:14 UTC
  • Mtaalamu: Hizbullah itaibuka mshindi katika vita vyovyote na Israel

Uwezo wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon katika nyuga tofauti zikiwemo za kijeshi, vita stadi na vita vya kisaikolojia umeutia kiwewe utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kiasi cha kuwafanya weledi wa masuala ya kivita kusema kwamba, vita vyovyote vitakavyojiri kati ya Israel na harakati hiyo, vitamalizika kwa ushindi wa Hizbullah.

Muhammad Ali Jafar, mtaalamu wa masuala ya kistratijia katika mtandao wa habari wa al-Ahdi nchini Lebanon ameandika kwamba, kuongezeka uwezo wa hali ya juu wa harakati hiyo ya Kiislamu sambamba na kuwa na stratijia mpya ni jambo lililozidisha wasi wasi na wahka mkubwa kwa utawala wa Kizayuni.

Wanamuqawama wa Hizbullah wakiwa wameubeba moja ya mwili wa shahidi

Kwa mujibu wa Jafar, stratijia hizo zinazotumiwa hivi sasa na Hizbullah zinabadili nukta dhaifu kuwa fursa zenye umuhimu kwa ajili ya kukabiliana na adui. Aidha mtaalamu huyo wa masuala ya kistratijia ameelezea namna ambavyo taswira ya harakati ya Hizbullah inavyoogopesha katika fikra za utawala wa Kizayuni kutokana na uwezo wake mkubwa wa kijeshi. Muhammad Ali Jafar amebainisha kwamba harakati hiyo inaendesha vita kupitia stratijia yenye nguvu na akili na kwa mujibu wa viwango vya kijeshi vya kisasa, licha ya jeshi la Israel kutumia kiwango cha juu cha teknolojia yake, lakini Hizbullah imefanikiwa kugeuza uwezo wa jeshi la utawala huo na kuwa nukta ya udhaifu.

Askari wa utawala wa Kizayuni wakilia baada ya kuadhibiwa na Hizbullah katika vita vya siku 33 mwaka 2006

Amezidi kufafanua kuwa, tatizo la Israel halipo kwenye namna ya kukabiliana na uwezo wa makombora ya Hizbullah, bali lipo kwenye uwezo wa kistratijia ambao harakati hiyo inaumiliki kwa sasa. Katika vita vya siku 33 kati ya Israel na wanamuqawama wa Hizbullah vilivyoanza mwezi Julai mwaka 2006 na kumalizika tarehe 14 mwezi Agosti mwaka huo huo, harakati hiyo ya Kiislamu iliibuka mshindi.