Maelfu waandamana Tel Aviv kupinga ubaguzi wa Israel
Watu zaidi ya elfu saba wamefanya maandamano katika barabara za mji wa Tel Aviv kupinga muswada wa kibaguzi wa utawala haramu wa Israel.
Waandamanaji hao wakiwemo wanasiasa, wanaharakati wa kijamii na wabunge Waisraeli walifanya maandamano haya jana Jumamosi kuonesha upinzani wao kwa muswada wa sheria inayotaka kutambuliwa Israel kama 'dola la Mayahudi pekee'.
Muswada huo unatazamiwa kupigiwa kura katika kikao cha kesho cha bunge la utawala wa Kizayuni wa Israel (Knesset).
Muswada huo unazifadhilisha 'thamani za Kizayuni' badala ya 'thamani za kidemokrasia' katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel.
Aidha muswada huo unautambua Quds kama mji mkuu wa Israel, kutaka kutambuliwa jamii ya Wayahudi pekee katika ardhi hizo za Palestina, sanjari na kukitambua Kiebrania kama lugha rasmi na kukitweza Kiarabu.
Taarifa ya waandaaji wa maandamano ya jana mjini Tel Aviv inasema, "Sheria hiyo iwapo itapasishwa, itaufanya ubaguzi, ujamii na utengano kama sehemu ya kila siku ya maisha yetu."