Saudia kukata msaada wa kujikimu kimaisha kutokana na matatizo ya kiuchumi
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i60924-saudia_kukata_msaada_wa_kujikimu_kimaisha_kutokana_na_matatizo_ya_kiuchumi
Kufuatia kushtadi matatizo ya kiuchumi, serikali ya Saudi Arabia imeongeza kiwango cha kodi na kukatisha ruzuku ya kimaisha nchini humo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
May 11, 2020 22:10 UTC
  • Saudia kukata msaada wa kujikimu kimaisha kutokana na matatizo ya kiuchumi

Kufuatia kushtadi matatizo ya kiuchumi, serikali ya Saudi Arabia imeongeza kiwango cha kodi na kukatisha ruzuku ya kimaisha nchini humo.

Mohammed Al-Jadaan, Waziri wa Fedha wa Saudia amesema kwamba kuanzia mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu kodi itaongezwa kutoks asilimia 5 hadi 15. Kadhalika ameongeza kuwa, kuanzia mwanzoni mwa mwezi huo, msaada wa kujikimu kimaisha utasitishwa pia. Waziri wa Fedha wa Saudia amesisitiza kwamba uamuzi huo umechukuliea kwa lengo la kusaidia kuimarisha uchumi wa nchi na kuchangia katika  kutatua matatizo ambayo hayajawahi kushuhudiwa nchini humo, yaliyosababishwa na virusi vya Corona na ili kwa uchache iweze kufidia hasara inayotokana na matatizo ya kifedha na kiuchumi hasa baada ya kushuka kwa kiasi kikubwa bei ya mafuta duniani.

 Mohammad Bin Salman, Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudia

Wiki iliyopita serikali ya Saudia pia sambamba na kupitisha muswada, ilitangaza kwamba ili kukabiliana na mazingira magumu yaliyosababishwa na kuenea kwa virusi vya Corona na kushadidi mgogoro wa kiuchumi nchini humo, inapunguza mishahara ya wafanyakazi katika sekta binafsi kwa asilimia 40. Saudi Arabia ambayo ni kati ya nchi zinazouza mafuta kwa wingi duniani na kutokana na kupenda kwake makubwa Mohammad Bin Salman, Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa nchi hiyo katika kuanzisha vita vya kichokozi dhidi ya Yemen na pia kuingia katika mzozo wa bei ya mafuta na Russia, imekumbwa na mgogoro mkubwa wa kifedha na kiuchumi kwa namna ambayo haijawahi kushuhudiwa.