Asia Magharibi
  • HAMAS yaisihi dunia: Msiiache Ghaza 'inayovuja damu' iyakabili 'mauaji ya halaiki' peke yake

    HAMAS yaisihi dunia: Msiiache Ghaza 'inayovuja damu' iyakabili 'mauaji ya halaiki' peke yake

    Mar 20, 2025 23:56

    Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa ombi la kuchukuliwa hatua za haraka kukomesha "uangamizaji kizazi wa kimpangilio unaofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel na kuwatesa kwa njaa makusudi Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza", jinai ambazo imesema, "zinafanywa kwa usaidizi wa kuaibisha wa kimaitaifa usioweza kuhalalishwa".

  • Tajiri maarufu wa US ashangaa mataifa ya Kiarabu kushindwa kuzuia mauaji ya kimbari Ghaza

    Tajiri maarufu wa US ashangaa mataifa ya Kiarabu kushindwa kuzuia mauaji ya kimbari Ghaza

    Mar 20, 2025 23:53

    Mohamed Hadid, mfanyabiashara tajiri, ambaye ni Mmarekani mwenye asili ya Palestina amehoji na kushangaa kwa nini mataifa ya Kiarabu na Kiislamu hayaingilii kati kukomesha mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.

  • Waziri wa zamani wa vita wa Israel: Tunakabiliwa na 'mgogoro mkubwa zaidi katika historia yetu'

    Waziri wa zamani wa vita wa Israel: Tunakabiliwa na 'mgogoro mkubwa zaidi katika historia yetu'

    Mar 20, 2025 23:52

    Waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel Moshe Ya'alon ametoa mwito kwa waandamanaji kuendeleza maandamano yao ili kuiangusha serikali ya Benjamin Netanyahu na kuhitimisha alichokiita 'mgogoro mkubwa zaidi katika historia ya Israel'.

  • Makundi ya muqawama yasisitiza kuunganisha juhudi ili kukabiliana na mashambulizi ya Israel

    Makundi ya muqawama yasisitiza kuunganisha juhudi ili kukabiliana na mashambulizi ya Israel

    Mar 20, 2025 07:00

    Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) na Harakati ya Wananchi kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina (PFLP) zimesisitiza juu ya haja ya kuunganisha juhudi makundi ya muqawama ya Palestina na nchi za Kiarabu ili kukabiliana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni na kuunga mkono mapambano ya ukombozi katika Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza na kupinga mipango ya Marekani na utawala wa Kizayuni ya kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina.

  • Israel yaua watu wengine 71 katika mashambulizi dhidi ya Gaza na kuikalia tena Netzarim

    Israel yaua watu wengine 71 katika mashambulizi dhidi ya Gaza na kuikalia tena Netzarim

    Mar 20, 2025 06:56

    Ripoti zinaonyesha kuwa ndani ya saa 24 zilizopita wanajeshi wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina zaidi ya 71 katika miji ya Beit Lahiya, Rafah na Khan Yunis, huku wengine wengi wakijeruhiwa.

  • Moto mpya wa vita wawashwa na utawala wa Kizayuni huko Gaza kwa msaada wa Marekani

    Moto mpya wa vita wawashwa na utawala wa Kizayuni huko Gaza kwa msaada wa Marekani

    Mar 20, 2025 06:22

    Kwa kukiuka makubaliano ya usitishaji vita huko Ghaza yaliyoanza kutekelezwa tarehe 19 Januari, utawala wa Kizayuni umeanzisha tena vita vya umwagaji damu dhidi ya eneo hilo lililoharibiwa na vita, kwa kufanya mashambulizi makubwa ya kinyama ambayo yamesababisha mauaji ya mamia ya mashahidi wa Kipalestina na kujeruhi wengine wengi katika ukanda huo.

  • San'a: Iran haiingilii hata chembe maamuzi ya Yemen

    San'a: Iran haiingilii hata chembe maamuzi ya Yemen

    Mar 20, 2025 03:13

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen amesisitiza kuwa: Iran haingilii hata chembe maamuzi ya serikali ya San’a na kwamba operesheni za Yemen dhidi ya Wazayuni ni uamuzi huru na utaendelea kutekelezwa kivitendo hadi mzingiro wa Ghaza utakapovunjwa kikamilifu.

  • Saudia: Israel inahatarisha usalama na utulivu wa eneo zima

    Saudia: Israel inahatarisha usalama na utulivu wa eneo zima

    Mar 20, 2025 03:12

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudia imesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unatishia usalama na utulivu wa eneo hili zima na kwamba jamii ya kimataifa na Baraza la Usalama zina wajibu wa kutekeleza majukumu yao ipaswavyo na kusimama kidete kukabiliana na hujuma za Israel huko Palestina na Syria.

  • Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu

    Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu

    Mar 19, 2025 23:40

    Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kushadidi mashambulio mabaya dhidi ya Gaza, akionya kwamba mashambulizi ya hivi karibuni ya anga, ambayo yaliua watoto wasiopungua 174 katika ukanda huo, ni mwanzo tu wa uchokozi mkubwa zaidi dhidi ya Wapalestina.