Lavrov ataka kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya Khashoggi
https://parstoday.ir/sw/news/world-i48949-lavrov_ataka_kuharakishwa_uchunguzi_kuhusu_mauaji_ya_khashoggi
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesisitiza ulazima wa kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya mwandishi habari mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Oct 21, 2018 11:09 UTC
  • Lavrov ataka kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya Khashoggi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesisitiza ulazima wa kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya mwandishi habari mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia.

Akizungumza katika mahojiano na televisheni ya Euro-News, Sergei Lavrov  ameashiria masuala yanayohusiana na mauaji ya Jamal Khashoggi mwandishi wa habari aliyekuwa akiukosoa utawala wa kifalme wa Saudia na kusisitiza kuwa Moscow inaunga mkono maombi ya kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya mwandishi huyo. 

Jamal Khashoggi, mwandishi habari aliyeuawa katika ubalozi mdogo wa Saudia nchini Uturuki

Alexei Pouchkov Mkuu wa Kamisheni ya Siasa ya Baraza la Russia pia amebainisha kuwa kadhia ya mauaji ya Khashoggi yaliyofanywa katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul Uturuki ni mfano wa wazi wa siasa za undumakuwili za Marekani. 

Alexei Pouchkov 

Pouchkov ameongeza kuwa serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani inafanya kila iwezalo kustafidi na kila hatua ili kulinda mikataba mikubwa ya uuzaji silaha baina yake na Saudi Arabia hata baada ya mauaji hayo ya kinyama ya Jamal Khashoggi; japokuwa si jambo rahisi kwa Marekani kulinda uhusiano wake na Saudia baada ya kuuliwa mandishi huyo wa habari aliyekuwa akiikosoa Saudia.