23
Akhlaqi Katika Uislamu (23)
Amani ya Allah, rehma na baraka zake ziwe juu yako mpendwa msikilizaji popote pale ulipo wakati huu. Nakukaribisha kusikiliza sehemu hii ya 23 ya kipindi cha Akhlaqi Katika Uislamu nikiwa na matumaini kuwa, mimi pamoja na wewe tutanufaika na yale tutakayoyasikia katika kipindi hiki ambacho kwa leo kitazungumzia sifa muhimu ya utamaduni mkwasi wa Uislamu ya kukataa madhila, kudunishwa na kudhalilishwa. Endelea kuwa nami basi hadi tamati ya mazungumzo yetu.