-
Rais wa Iran na Waziri Mkuu wa Iraq wafanya mkutano na waandishi wa habari Baghdad
Sep 11, 2024 23:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mkutano na waandishi wa habari akiwa pamoja na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Iraq: "tunapaswa kutekeleza makubaliano ya ushirikiano wa kiusalama kati ya Iran na Iraq ili kukabiliana na magaidi na maadui".
-
Shahram Irani: Iran haiogopi kukabiliana na dola lolote
Sep 10, 2024 03:36Kamanda wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa nchi hii imefikia kiwango cha nguvu za aina yake ambazo zinaifanya iweze kuchukua hatua mkabala wa hujuma na makabiliano mbalimbali dhidi yake.
-
Iran: Hatuna nafasi yoyote katika vita vya Russia na Ukraine
Sep 08, 2024 08:34Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haina mchango wowote katika vita vinavyoendelea kati ya Russia na Ukraine, na daima imekuwa ikikariri wito wake wa mazungumzo ya kuutafutia ufumbuzi mzozo huo.
-
Rais Pezeshkian wa Iran kuitembelea Iraq katika ziara ya kwanza nje ya nchi
Sep 08, 2024 08:05Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian anatazamiwa kuitembelea Iraq siku ya Jumatano katika safari yake ya kwanza ya nje tangu aingie madarakani.
-
Araghchi asisitiza kuimarishwa uhusiano wa Iran na Serbia
Sep 07, 2024 03:49Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesitiza umuhimu wa kutumia rasilimali zote zilizopo ili kuimarisha uhusiano kati ya Iran na Serbia, hasa katika sekta ya uchumi.
-
Maghala ya nyuklia ya Israel tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia
Sep 06, 2024 23:00Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa kikanda na wa ulimwengu mzima.
-
Sera ya kuunga mkono Palestina, kipaumbele cha serikali ya 14
Sep 06, 2024 09:13Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuunga mkono muqawama wa wananchi wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel ni moja ya vipaumbele vya serikali ya 14 na sehemu muhimu ya nguzo za siasa za nje za Iran.
-
Naibu Kamanda wa IRGC: Jibu la Iran kwa mauaji ya Haniyeh litakuwa 'tofauti, la kushangaza' na la wakati muafaka'
Sep 04, 2024 23:03Naibu Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ameonya kuwa jibu la Tehran kwa mauaji ya Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas aliyeuawa kigaidi mjini Tehran, litakuwa tofauti na la kushangaza.
-
Wairan waghariki katika kumbukizi ya kuuawa shahidi Imam Ridha AS
Sep 04, 2024 03:32Wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran tokea jana usiku wamezama katika maombolezo ya kukumbuka kuuawa shahidi Imam Ali Ridha (AS), mjukuu wa Mtume Mtukufu (SAW) miaka 1242 iliyopita.
-
Iran yawaita mabalozi wa UK, Australia mjini Tehran
Sep 04, 2024 03:30Balozi wa Uingereza mjini Tehran ameitwa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran na kukabidhiwa malalamiko ya Jamhuri ya Kiislamu, baada ya serikali ya London kuwawekea vikwazo shakhsia watatu Wairan na taasisi moja ya Iran.