-
Watu 13 wauawa katika mashambulio ya wanamgambo wa ADF huko DRC
Oct 12, 2021 04:38Watu wasiopungua 13 wameuawa katika eneo la Oicha mkoa wa Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kufuatia mashambulio ya waasi wa Uganda wa ADF.
-
Watu wasiopungua 30 wauawa katika shambulio kaskazini mashariki mwa Kongo
Sep 06, 2021 20:52Duru za habari za kieneo na Umoja wa Mataifa jana Jumatatu ziliarifu kuwa, watu wasiopungua 30 waliuliwa katika shambulio la siku ya Jumaosi kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Maelfu ya watu wakumbwa na tatizo la kuhara baada ya maji ya mto kuchafuka, Kongo
Aug 31, 2021 22:22Maafisa wa afya katikka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameripoti kuwa, maelfu ya watu wamepatwa na tatizo la kuhara katika jimbo la Kasai katikati mwa nchi hiyo baada ya raia kutumia maji machafu na samaki waliokufa kutoka katika ziwa ambalo maji yake yamechafuka.
-
Ripoti: Raia 450 wameuawa DRC kati ya Januari na Julai 2021
Aug 24, 2021 03:25Shirika moja la kiraia katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limesema mamia ya raia wameuawa ndani ya miezi saba ya kwanza ya mwaka huu 2021.
-
Watu kadhaa wauawa na waasi wa ADF mjini Beni, Kongo DR
Aug 12, 2021 03:38Watu wasiopungua watatu wameuawa huku wengine kadhaa wakijeruhiwa katika shambulizi la waasi wa kundi la ADF katika eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Makumi wapoteza maisha katika ajali ya barabarani Kongo DR
Aug 02, 2021 22:46Makumi ya watu wamepoteza maisha katika ajali mbaya ya barabarani iliyotokea huko magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Wanachuo waandamana Kongo kupinga kuuliwa mwenzao kwa kutovaa barakoa
Jul 27, 2021 03:17Wanafunzi wa Chuo Kikuu mjini Kinshasa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameendelea kuandamana kulalamikia kitendo cha polisi cha kumuua mwanachuo mwenzao kwa madai ya kutovaa barakoa ya kujikinga na maambukizi ya corona.
-
Mafuriko yasababisha maafa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Jul 17, 2021 07:52Mafuriko yaliyotokea kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 16.
-
Congo DR yaweka kafyu katika mji wa Beni baada ya milipuko ya mabomu kanisani
Jun 28, 2021 06:17Wakazi wa mji wa Beni nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo Jumatatu wamekumbana na zuio la kafyu katika mji huo baada ya milipuko mitatu ya mabomu kutokea katika mji huo. Maafisa wametahadharisha kuwa, wana taarifa kwamba milipuko mingine zaidi inaratibiwa.
-
Mamia ya wakimbizi wa Kongo DR wamiminika Uganda
Jun 16, 2021 21:59Wakimbizi karibu elfu moja raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamewasili nchini Uganda katika kipindi cha siku chache zilizopita.