-
Israel iliteka nyara Wapalestina 500 mwezi Machi
Apr 11, 2017 02:01Utawala wa Kizayuni wa Israel uliwateka nyara Wapalestina 509 katika Ukanda wa Ghaza, Ukingo wa Magharibi na Quds Tukufu mwezi uliopita wa Machi.
-
Jumuiya ya Wafanyakazi Norway yataka kutambuliwa rasmi nchi ya Palestina
Apr 08, 2017 22:10Jumuiya ya Wafanyakazi nchini Norway imetoa wito wa katambulwia rasmi nchi huru ya Palestina.
-
Brazil yalaani ujenzi mpya wa nyumba za Mayahudi Ukingo wa Magharibi
Apr 05, 2017 03:17Brazil imelaani uamuzi uliopasishwa hivi karibuni na baraza la mawaziri la utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
EU: Hatutohamishia balozi zetu Quds tukufu kutoka Tel Aviv
Apr 04, 2017 11:21Katika hali ambayo Marekani imezungumzia mpango wa kuhamishia ubalozi wake ulioko Israel kutoka Tel Aviv na kuupeleka katika mji wa Quds tukufu huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, Umoja wa Ulaya umesema nchi wanachama wake hazitofuata sera hizo za Washington.
-
UN: Jamii ya kimataifa ichukue hatua za dhati kukomesha kukaliwa kwa mabavu Palestina
Apr 03, 2017 09:33Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu huko Palestina amesema kuwa, jamii ya kimataifa ina wajibu wa kuchukua hatua nyingi zaidi mbali ya maazimio na kutoa taarifa tu ili kukomesha kukaliwa kwa mabavu Palestina na ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Hati mpya ya Kisiasa ya HAMAS: Wakimbizi wa Kipalestina warejee kwenye ardhi zao za asili
Apr 03, 2017 03:14Baadhi ya vifungu vya hati mpya ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS vimetangazwa vikisisitizia haki ya wakimbizi wote wa Kipalestina walioko maeneo tofauti duniani kurejea kwenye ardhi zao za asili.
-
Mayahudi waandamana Quds kulaani ukaliaji wa mabavu wa Palestina
Apr 02, 2017 03:36Maelfu ya Mayahudi wamefanya maandamano katika eneo la Quds tukufu kulaani upanuzi wa vitongoji vya walowezi za Kizayuni katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Israel inakalia kwa mabavu asilimia 85 ya ardhi za Palestina
Mar 30, 2017 02:21Utawala wa Kizayuni wa Israel unakalia kwa mabavu asilimia 85 ya ardhi zote za Wapalestina.
-
Wamarekani waandamana Washington dhidi ya lobi ya Kizayuni
Mar 27, 2017 03:16Wanaharakati wanaounga mkono Palestina wamefanya maandamano nje ya ukumbi kunakofanyika kongamano la lobi ya Kizayuni ya Kamati ya Marekani na Israel ya Masuala ya Umma (AIPAC) mjini Washington.
-
Askari wa Israel wamuua shahidi kijana mwengine Mpalestina, ujenzi wa vitongoji waongezeka kwa asilimia 40
Mar 24, 2017 00:00Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameishambulia kwa risasi gari moja kaskazini mwa Ramallah katika Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan na kupelekea kuuawa shahidi kijana mmoja Mpalestina na kujeruhiwa wengine watatu.