-
Katibu Mkuu wa UN atoa indhari ya uwezekano wa kufanyika jinai kubwa Sudan Kusini
Nov 17, 2016 04:04Katibu Mkuu wa Umoja w Mataifa ametoa indhari kuhusu uwezekano wa kufanyika jinai kubwa nchini Sudan Kusini.
-
UN yatadharidha kutokea mauaji ya kimbari Sudan Kusini
Nov 12, 2016 04:16Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa ameonya kuwa yumkini Sudan Kusini ikatumbukia katika mauaji ya kimbari kutokana na kushadidi mapigano ya kikabila nchini humo.
-
Kenya yaanza kuondoa askari wake wa kulinda amani Sudan Kusini
Nov 10, 2016 00:08Kundi la kwanza la askari wa Kenya waliokuwa wakihudumu katika operesheni ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) walirejea nchini mwao hapo jana baada ya serikali ya Nairobi kuwaamuru waondoke nchini humo kufuatia kutimuliwa kamanda wa Kenya aliyekuwa akiongoza operesheni hiyo.
-
Machar aikosoa Kenya kwa kumtimua msemaji wake
Nov 05, 2016 00:06Kiongozi wa waasi nchini Sudan Kusini ameijia juu serikali ya Kenya kwa kumtimua nchini humo msemaji wake James Gatdet Dak na kusisitiza kuwa hatua hiyo imekiuka Hati ya makubaliano ya Geneva.
-
Uhuru: Kenya haijutii kuwaondoa wanajeshi wake Sudan Kusini
Nov 03, 2016 12:57Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema taifa hilo halijuti kwa uamuzi wake wa kuwaondoa wanajeshi wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki walioko Sudan Kusini chini ya mwavuli wa kikosi maalumu cha kusimamia amani cha Umoja wa Mataifa (UNMISS).
-
Umoja wa Mataifa wakiri vikosi vyake kushindwa kuwalinda raia Sudani Kusini
Nov 02, 2016 04:32Umoja wa Mataifa umetangaza na kukiri kwamba, vikosi vyake vya kulinda amani huko Sudani Kusini vilishindwa kuwalinda raia katika mji mkuu Juba wakati wa mapigano baina ya pande mbili mwezi Julai mwaka huu.
-
Kuongezeka vitendo vya utumiaji mabavu na ukatili nchini Sudan Kusini
Oct 31, 2016 01:11Katika hali ambayo asasi za kimataifa zinafanya juhudi za kuhitimisha vitendo vya ukatili nchini Sudan Kusini, bado wimbi la vitendo hivyo vingali vinaendelea nchini humo.
-
Zaidi ya watoto 100 wanaotumika vitani Sudan Kusini wakombolewa
Oct 27, 2016 01:59Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza habari ya kukombolewa zaidi ya watoto wadogo 100 waliokuwa wanatumika vitani nchini Sudan Kusini.
-
Salva Kiir awaonya wafanyao fujo Sudan Kusini
Oct 24, 2016 00:29Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amewaonya wafanyao fujo na wanaozusha machafuko ya kikabila nchini humo.
-
UN: Makampuni ya Silaha ya Israel yanachochea vita Sudan Kusini
Oct 21, 2016 04:36Jopo la Umoja wa Mataifa limepata ushahidi wa kuwepo mitandao ya silaha yenye makazi Israel na Ulaya Mashariki ambao inachochea vita vinavyoendelea sasa huko Sudan Kusini.