-
Wanafunzi 6 na mlinzi wauawa baada ya shule kuvamiwa na maharamia Kenya
Oct 14, 2017 09:36Kwa akali wanafunzi sita na bawabu wa shule moja katika mji wa Lokichogio, kaskazini mwa Kenya wameuawa baada ya shule yao kuvamiwa na maharamia wanaoaminika kutoka Sudan Kusini, usiku wa kuamkia leo.
-
17 wapoteza maisha baada ya moto kuteketeza misitu, makazi Marekani
Oct 11, 2017 08:17Watu wasiopungua 17 wamefariki dunia katika mkasa wa moto unaoendelea kuteketeza misitu katika jimbo la California nchini Marekani.
-
Watu 100 wameuawa katika machafuko ya hivi karibuni nchini Cameroon
Oct 06, 2017 14:20Mtandao wa watetezi wa haki za binaadamu katikati mwa Afrika umetangaza kuwa, jumla ya watu 100 waliuawa katika machafuko yaliyoibuka hivi karibuni katika maeneo mawili ya watu wanaozungumza lugha ya Kingereza nchini Cameroon.
-
Wanamgambo 10 wauawa katika mapigano na jeshi la Kongo DR
Oct 05, 2017 14:03Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetangaza habari ya kuuawa wanamgambo 10 katika mapigano na jeshi la nchi hiyo.
-
Shambulizi la anga la Marekani laua raia 45 nchini Syria
Oct 03, 2017 08:14Kwa akali raia 45 wameuawa katika shambulizi la anga la hivi punde lililotekelezwa na ndege za kivita za Marekani nchini Syria.
-
Watu 58 wauawa katika hujuma ya kigaidi Las Vegas, Marekani
Oct 02, 2017 14:25Watu 58 wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika hujuma ya kigaidi iliyotekelezwa katika mji wa Las Vegas nchini Marekani ambayo imetajwa kuwa tukio mbaya zaidi la ufyatuaji risasi kiholela nchini humo.
-
224 waaga dunia katika mtetemeko wa ardhi nchini Mexico
Sep 20, 2017 13:47Kwa akali watu 224 wamepoteza maisha kutokana na mtetemeko mkubwa wa ardhi ulioikumba Mexico, ikiwa ni chini ya wiki mbili baada ya zilzala nyingine kuua makumi ya watu nchini humo.
-
Serikali ya Kongo DR yaanza uchunguzi kuhusu mauaji ya wakimbizi wa Burundi
Sep 18, 2017 14:09Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema kuwa imeanza kuchunguza mauaji ya makumi ya wakimbizi wa Burundi waliouliwa nchini humo.
-
Mapigano yapamba moto kaskazini magharibi mwa Libya
Sep 18, 2017 04:01Mapigano makali yamepamba moto kati ya makundi hasimu katika mji wa Misrata wa kaskazini magharibi mwa Libya. Mtu mmoja ameuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa.
-
Mapigano mapya yaibuka kati ya wanamgambo wa Seleka nchini CAR
Sep 09, 2017 16:27Duru za usalama nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati zimeripoti habari ya kujiri mapigano mapya kati ya waasi wa zamani wa kundi la Seleka katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo.