-
Watatu wauawa Zimbabwe, askari usalama wapambana na wapinzani wanaopinga matokeo ya uchaguzi
Aug 02, 2018 08:07Polisi ya Zimbabwe imesema watu watatu waliuawa jana wakati askari walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa upinzani waliokuwa wakirembea mawe huku wakikituhumu chama tawala cha Zanu-PF kuwa kinajaribu kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliofanyika siku ya Jumatatu.
-
Askari wapambana na wafuasi wa upinzani Zimbabwe huku ZANU-PF ikipata ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa bunge
Aug 01, 2018 16:37Milio ya risasi ya bunduki za otomatiki imesikika katika mitaa ya mji mkuu wa Zimbabwe, Harare leo wakati askari walipoingilia kati kuwatawanya waandamanaji waliopambana na polisi baada ya kiongozi mkuu wa upinzani kukituhumu chama tawala cha Zanu-PF kuwa kinajaribu kuyachakachua matokeo ya uchaguzi.
-
Mnangagwa na Chamisa wasema wana matumaini ya kushinda uchaguzi wa Rais Zimbabwe
Jul 31, 2018 15:58Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na mgombea wa chama cha MDC, Mchungaji Nelson Chamisa wamesema wote kuwa wana matumaini ya kushinda katika uchaguzi wa rais uliofanyika jana nchini humo.
-
Uchaguzi wa Rais Zimbabwe waanza, Mugabe akipa mgongo chama tawala
Jul 30, 2018 08:16Mamilioni ya wananchi wa Zimabwe wameelekea kwenye masanduku ya kupigia kura katika uchaguzi wa kwanza wa rais ambao haumshirikishi kiongozi mkongwe wa nchi hiyo, Robert Mugabe tangu Zimbabwe ipate Uhuru mwaka 1980.
-
UN: Wapiga kura wanatishiwa Zimbabwe kuelekea uchaguzi mkuu
Jul 24, 2018 16:24Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeelezea wasiwasi mkubwa ilionao kuhusu kukithiri visa vya wapiga kura kutishiwa maisha nchini Zimbabwe, baadhi yao wakilazimishwa kushiriki mikutano wa kisiasa, zikiwa zimesalia siku chache wananchi waelekee katika masanduku ya kupigia kura kuwachagua viongozi wao.
-
Mnangagwa: Wakulima wazungu wasiwe na hofu kuhusu ardhi zao
Jul 22, 2018 07:23Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amewafahamisha wakulima wazungu nchini humo kuwa zama za kuchukuliwa kwa nguvu ardhi zao zimemalizika huku akiwataka wafanye kazi pamoja na serikali yake.
-
Maandamano dhidi ya chama tawala yafanyika Zimbabwe
Jul 12, 2018 04:11Maelfu ya wafuasi wa upinzani jana Jumatano walijitokeza mabarabarani kushiriki maandamano dhidi ya chama tawala nchini Zimbabwe Zanu-pf katika mji mkuu Harare.
-
Washukiwa wawili watiwa nguvuni kuhusiana na mlipuko wa Zimbabwe
Jul 04, 2018 13:55Polisi nchini Zimbabwe imewatia mbaroni washukiwa wawili kuhusiana na mlipuko wa guruneti ulioua watu wawili na kuwajeruhi wengine 47 katika mkutano wa kampeni wa Rais Emmerson Mnangagwa mwezi uliopita.
-
Mnangagwa ailaumu G40 inayomuunga mkono Grace Mugabe kwa mripuko
Jun 28, 2018 03:31Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema anashuku huenda kundi la G40 linalomuunga mkono Grace Mugabe, mke wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo ndilo lililohusika katika kile anachokitaja kama jaribio la mauaji dhidi yake katika mji wa Bulawayo Jumamosi iliyopita.
-
Polisi nchini Zimbabwe yamtia mbaroni kiongozi wa upinzani
Jun 26, 2018 15:28Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe amekamatwa na polisi ya nchi hiyo baada ya kushinikiza kujiuzulu kwa mkuu wa Tume ya Uchaguzi, mwezi mmoja kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu nchini humo.