-
Angola imempa hifadhi Rais wa zamani wa Gabon Ali Bongo aliyefukuzwa madarakani
May 16, 2025 23:17Rais wa zamani wa Gabon Ali Bongo na familia yake wameachiwa kutoka kizuizi cha nyumbani na kuhamishiwa Angola. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Ijumaa na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Joao Lourenco.
-
Kuporomoka ushawishi wa Ufaransa Afrika Kaskazini
May 16, 2025 22:50Kufuatia kuongezeka mvutano wa kidiplomasia kati ya Ufaransa na Algeria, Paris imechukua uamuzi wa kuwafukuza wanadiplomasia wa Algeria walio na hati za kusafiria za kidiplomasia zisizo na visa kujibu mapigo kwa uamuzi wa Algeria wa kuwafukuza wanadiplomasia 15 wa Ufaransa.
-
Umeme wakatika kikamilifu Khartoum kutokana na mashambulizi ya droni za RSF
May 16, 2025 06:48Shirika la Umeme la Sudan alisema kuwa, vituo viwili vya kuzalisha umeme vimeshambliwa kwa droni (ndege zisizo na rubani) za Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) na kusababisha kuwaka moto na kukatika umeme katika mji mkuu.
-
Kadhaa wauawa katika shambulio la droni kusini ya Sudan
May 16, 2025 03:36Watu kadhaa wameripotiwa kuuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa, baada ya ndege isiyo na rubani kushambulia hospitali moja katika mji wa El-Obeid, mji mkuu wa Jimbo la Kordofan Kaskazini kusini mwa Sudan jana Alkhamisi.
-
Watoto nusu milioni waingia hatarini kutoka na ghasia mjini Tripoli Libya
May 15, 2025 22:52Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limesema kuwa, kuongezeka ghasia ndani na karibu na mji mkuu wa Libya, Tripoli, kunatishia usalama wa karibu watoto nusu milioni mjini humo.
-
Rais wa zamani wa Mauritania aongezewa kifungo, sasa ni miaka 15 jela
May 15, 2025 22:51Mahakama ya rufaa ya Mauritania imemhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo, Mohamed Ould Abdel Aziz kifungo cha miaka 15 jela kwa tuhuma za ubadhirifu, matumizi mabaya ya madaraka na utakatishaji fedha.
-
DRC yatishia kuweka vikwazo vikali zaidi vya mauzo ya madini adimu ya cobalt
May 15, 2025 22:48Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema kuwa inaweza kuweka vikwazo vikali zaidi vya mauzo ya cobalt wakati marufuku yake ya miezi minne itakapomalizika.
-
Wakuu wa ujasusi watembelea Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance. Kulikoni?
May 15, 2025 07:58Katika hatua ya kwanza ya aina yake, wakuu wa mashirika ya ujasusi na usalama kutoka nchi za Afrika Mashariki wametembelea Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD) magharibi mwa Ethiopia.
-
Uzinduzi wa chama kipya cha Gachagua wavurugwa na walioitwa "wahuni", Kenya
May 15, 2025 07:27Hafla ya uzinduzi wa chama kipya cha aliyekuwa Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua, cha Democracy for the Citizens Party (DCP) zimevurugwa mapema leo Alkhamisi baada ya kuingiliwa na watu waliotajwa na vyombo vya habari nchini humo kuwa ni "wahuni".
-
Al-Qaeda yatangaza kuhusika na mashambulizi ya Burkina Faso, yasema imeua wanajeshi 60
May 15, 2025 07:26Kundi lenye mafungamano na al-Qaeda, JNIM, limetangaza kuhusika na shambulio lililofanyika katika eneo la kijeshi kwenye jimbo la Loroum kaskazini mwa Burkina Faso, likidai kuwaua wanajeshi 60.