-
Kamanda Mkuu wa jeshi la Iran: Kuendelea serikali ya Netanyahu ni kuendeleza vita Ukanda wa Gaza
Apr 08, 2024 08:23Kamanda Mkuu wa jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kuendelea kuhudumu serikali ya Beanjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni kunafungamana na kuendelea vita huko Ukanda wa Gaza.
-
Leo ni siku ya Taifa ya Teknolojia ya Nyuklia nchini Iran
Apr 08, 2024 08:18Leo, Jumatatu tarehe 8 Aprili mwaka 2024, imepewa jina la "Siku ya Taifa ya Teknolojia ya Nyuklia" kwa kutambua juhudi kubwa za kujifakharisha za wanasayansi wa nyuklia wa Iran katika kukamilisha mzunguko wa nishati ya nyuklia.
-
Kiongozi Muadhamu awataka wanafunzi wawe na mtazamo wa ukosoaji
Apr 08, 2024 04:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameutaja mustakabali bora kuliko leo kuwa ndio lengo kuu la nchi na mfumo wa Kiislamu, na kutoa wito kwa wanafunzi na jumuiya za wanafunzi kuwasilisha masuluhisho mapya ili kufikia lengo na maendeleo haya ya kimsingi bila kudorora nchi kimaada na kimaanawi.
-
Iran ni kisiwa cha utulivu katika eneo la Asia Magharibi
Apr 08, 2024 02:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema Iran ni kisiwa cha utulivu na usalama katika eneo lenye matatizo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati).
-
Iran: Tunaunga mkono mwenendo wa mazungumzo ya amani huko Yemen
Apr 07, 2024 23:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaunga mkono mwenedo wa mazungumzo ya amani huko Yemen.
-
Qalibaf: Enzi ya ubabe wa Israel kwa himaya ya Marekani imekwisha
Apr 07, 2024 08:28Spika wa Bunge la Iran Mohammad Baqer Qalibaf amesema enzi za ubabe wa utawala wa Isarel kwa himaya ya Marekani katika eneo la Asia Magharibi zimepita na utawala huo unaelekea kuangamia.
-
Jenerali Baqeri: Shambulio la Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria lilikuwa 'kujiua'
Apr 06, 2024 23:28Kamanda wa ngazi ya juu wa jeshi la Iran amesema shambulizi la hivi karibuni la utawala ghasibu wa Israel dhidi ya vituo vya kidiplomasia vya Iran katika mji mkuu wa Syria, Damascus, ni sawa na kichaa na kujitia kitanzi utawala huo.
-
Aliyeongoza mashambulizi ya kigaidi kusini mashariki mwa Iran, atiwa mbaroni
Apr 06, 2024 07:05Msemaji wa Komandi Kuu ya Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza habari ya kutiwa mbaroni gaidi aliyeongoza mashambulizi ya kigaidi huko kusini mashariki mwa Iran. Gaidi huyo ametiwa mbaroni kwenye mji wa Karaj wa mkoa wa Alborz wa magharibi mwa Tehran.
-
Mtazamo wa wachambuzi wa mambo kuhusu mashambulio ya kigaidi kusini mashariki mwa Iran
Apr 06, 2024 03:39Mkoa wa Sistan na Baluchistan wa kusini mashariki mwa Iran, kwa mara nyingine tena umekumbwa na mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa na genge linaloungwa mkono na utawala wa Kizayuni wa Israel na Marekani.
-
Rais wa Iran: Walimwengu watajionea kuangamia kwa utawala wa Kizayuni
Apr 06, 2024 03:27Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu maalumu za kuwashukuru wananchi walio macho na wenye kujali thamani ya mambo wa Iran kwa ushiriki wao mkubwa katika matembezi ya Siku ya Quds Duniani na kusema: Walimwengu watajionea kuangamia kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.