-
Raisi: Iran ina ubunifu katika nyanja mbalimbali kwa ajili ya dunia
Apr 27, 2024 09:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika sherehe za ufunguzi wa maonyesho ya sita ya uwezo wa mauzo ya nje ya bidhaa za Iran (Iran Expo 2024) kwamba maonesho haya yanaonyesha kuwa Iran haiwezi kuwekewa vikwazo na ina uwezo wa kufanya uvumbuzi katika nyanja mbalimbali.
-
Wanafunzi wa Chuo Kikuu Tehran waandamana kuunga mkono maandamano ya wenzao wa Marekani
Apr 27, 2024 09:48Wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Tehran wamefanya maandamano leo Jumamosi kuunga mkono maandamano yanayoongezeka kwenye kampasi za Marekani ambapo wanafunzi wamepiga kambi wakitaka kukomeshwa vita vya Israel dhidi ya watu wa Gaza huko Palestina.
-
Iran Expo 2024, maonyesho ya uwezo wa kiuchumi wa Iran
Apr 27, 2024 07:13Maonesho ya sita ya uwezo wa kusafirisha nje bidhaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRAN EXPO 2024) yameanza leo mjini Tehran kwa lengo la kuonesha uwezo wa kiuchumi wa Iran.
-
Iran kuimarisha uhusiano wa kijeshi na Russia, China
Apr 27, 2024 04:41Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Brigadier Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amekutana na mawaziri wenzake wa ulinzi wa China na Russia kujadili njia za kuimarisha zaidi uhusiano wa kijeshi kwa ajili ya kuimarisha usalama na uthabiti duniani.
-
Raisi: Mtazamo wa Iran kuhusu Afrika ni wa kimkakati na unaozingatia maslahi ya pamoja
Apr 26, 2024 23:18Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaja mtazamo wa Iran kuhusu bara la Afrika kuwa ni wa kistratijia na unaozingatia maslahi ya pamoja na akasisitiza azma ya viongozi wa ngazi za juu wa nchi mbili za Iran na Zimbabwe ya kupanua na kuboresha kiwango cha ushirikiano.
-
Kikao cha Pili cha Kimataifa cha Iran na Afrika; nembo ya azma ya kupanua ushirikiano
Apr 26, 2024 11:07Kikao cha pili cha kimataifa kati ya Iran na Afrika kimefanyika leo asubuhi (Ijumaa) kwa kuhudhuriwa na maafisa wa ngazi za juu wa masuala ya kiuchumi wa nchi zaidi ya 30 za Afrika na kwa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika ukumbi wa mikutano wa nchi za Kiislamu mjini Tehran.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Vikosi vya ulinzi vya Iran ni mihimili imara mno ya taifa
Apr 26, 2024 08:37Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema: Vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni mihimili imara mno kwa taifa na inayoiletea dini izza na heshima.
-
Rais Raisi: Kuna irada ya kuimarisha uhusiano wa Afrika na Iran
Apr 26, 2024 04:40Raisi Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuna irada baina ya Iran na Afrika kuimarisha na kustawisha uhusiano wa kibiashara.
-
Damu ya mashahidi wa hujuma ya kigaidi ya Damascus iliufedhehesha utawala wa Kizayuni
Apr 26, 2024 04:30Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, damu safi ya mashahidi wa shambulio la kigaidi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, imeibua heshima na fahari kwa harakati za mapambano ya Kiislamu (muqawama) na kuufedhehsha utawala wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari.
-
Iran inatoa wito kwa BRICS kuchukua jukumu kukomesha jinai za Israel
Apr 26, 2024 04:23Iran imetoa wito kwa kundi la BRICS la mataifa yanayoinukia kiuchumi kuchukua jukumu la kukomesha mara moja jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina.