-
HAMAS: Badala ya mazungumzo mapya, Wazayuni walazimishwe kutekeleza usitishaji vita
Aug 13, 2024 02:10Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema utawala ghasibu wa Kizayuni umethibitisha kuwa hautaki kufikia makubaliano; na kwa sababu hiyo, harakati hiyo imewataka wapatanishi wa Misri na Qatar wawalazimishe Wazayuni watekeleze pendekezo la hivi karibuni la usitishaji vita badala ya kutaka yaanzishwe mazungumzo mengine mapya.
-
OIC yatakiwa kuunga mkono mhimili wa muqawama
Aug 12, 2024 23:07Mkuu wa Baraza la Maulamaa wa Nigeria amelaani vikali mashambulizi ya kigaidi ya hivi karibuni ya utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Waislamu wa Gaza, ambayo yalisababisha vifo vya watu karibu 200 walipokuwa wakiswali Swala ya alfajiri katika shule ya Tabeen.
-
Utawala wa Kizayuni, mbunifu wa mbinu mpya za mauaji ya kimbari
Aug 12, 2024 23:04Katika kitendo kingine cha jinai na uhalifu wa kutisha, utawala wa Kizayuni wa Israel umeshambulia shule ya al-Tabiin huko Gaza na kuuwa shahidi na kujeruhiwa mamia ya Wapalestina.
-
HAMAS: OIC na Arab League zifanye mkutano haraka ili kusimamisha mauaji ya kimbari ya Ghaza
Aug 12, 2024 07:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa wito kwa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) zifanye mkutano wa dharura wa kuchukua hatua dhidi ya mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wazayuni wazidi kujawa na hofu na kiwewe cha kungojea ulipizaji kisasi wa Mhimili wa Muqawama
Aug 12, 2024 07:35Utawala wa Kizayuni wa Israel umerefusha muda wa kuviweka katika hali ya tahadhari vikosi vya jeshi lake la anga kwa kuhofia madhara makubwa yatakayosababishwa na jibu la ulipizaji kisasi la Mhimil wa Muqawama kufuatia mauaji ya Ismail Haniya, aliyeuliwa shahidi na utawala huo wa kigaidi.
-
Hamas: Vita havitakwisha kama anavyotarajia adui Muisraeli
Aug 12, 2024 02:32Kiongozi wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amesema vita "havitakwisha kama anavyotarajia adui Muisraeli."
-
Hizbullah yashambulia kwa mafanikio kambi ya jeshi la Israel huko Giaton
Aug 12, 2024 02:23Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kwamba imeshambulia kwa mafanikio kambi muhimu ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika maeneo ya kaskazini yanayokaliwa kwa mabavu.
-
Maafisa wa jeshi la Israel wamepoteza matumaini ya kupata ushindi katika vita vya Ghaza
Aug 11, 2024 23:38Maafisa wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamekiri kuwa, ushindi dhidi ya Muqawama wa Palestina katika Ukanda wa Ghaza uko mbali sana kupatikana.
-
Ripota wa UN: Israel inafanya mauaji ya kimbari Gaza kwa silaha za US, Ulaya
Aug 11, 2024 04:05Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu amekosoa vikali hatua ya utawala wa Kizayuni ya kuendelea kufanya mauaji na jinai nyingine za kutisha dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
OIC yalaanii jinai mpya ya Israel na kutaka ilazimishwe kusitisha vita
Aug 11, 2024 02:14Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani jinai mpya ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza, na kusisitiza kuwa, utawala huo unapaswa kulazimishwa kuanzisha usitishaji vita mara moja.